Social Icons

Tuesday, September 27, 2011

TWANGA PEPETA, BI KIDUDE WAPAGAWISHA TAMASHA LA SANAA BAGAMOYOWanamuziki wa Bendi ya African Stars International 'Twanga Pepeta' wakiwajibika stejini hapo jana kwenye Tamasha la miaka 30 ya Sanaa na Utamaduni lililofunguliwa katika Ukumbi wa Sanaa Bagamoyo Pwani.
Mkongwe wa muziki wa Mwambao nchini Bi Kidude, akitumbuiza kwenye tamasha hilo usiku wa kuamkia leo.
Wanenguaji wa Bendi ya Twanga Pepeta wakiwajibika jukwaani hapo.
Kikundi cha Muziki wa Mwambao kilichokuwa kikitumbuiza na Bi Kidude.
Mrembo akipiga kinanda katika tamasha hilo.
Bi Kidude (kulia), akiokota fedha alizotunzwa na mashabiki wake wakati akiimba.
Wananamuziki hao wakiwajibika jukwaani.

Mmoja wa wanamuziki hao akiwajibika.

Bi Kidude (kushoto), akisalimiana na kiongozi wa wanamuziki wa Twanga Pepeta Luiza Mbutu (kulia), katika ni mmoja wa wanenguaji hao akifuatilia maongezi hayo.
Mwanamuziki wa Twanga Pepeta Mwijuma Mumini (kushoto), akisalimiana na Bi Kidude.
Kiongozi wa wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta Lilian Internet, akijitetea baada ya kubanwa mkono na Bi Kidude, baada ya kukawia kumsalimia.
Baadhi ya wanenguaji wa bendi hiyo wakiwa katika pozi.
Maria Soloma (kulia), akibadilishana mawazo na Sabrina Mathew kwenye chumba cha mapumziko.
Mpiga Drums wa Bendi hiyo Yahya Omar, akiwa katika moja ya jukum lake.
Mpiga gitaa la Bass wa bendi hiyo Kado, akijaribu kumchezea lafu mke wa mkuu wa wanenguaji wa bendi hiyo Super K.
Super K (kushoto), akimkoromea kiaina Kado baada ya kumkuta akichezea mali yake.
Muimbaji wa Twanga Pepeta Dogo Rama akiwajibika.

BENDI ya African Stars International ‘Twanga Pepeta, na Mkongwe wa muziki wa Mwambao Bi Kidude, usiku wa kuamkia leo walifanya makamuzi ya kufa mtu katika Tamasha la Miaka 30 ya Sanaa na Utamaduni lililoanza tangu Septemba 26 mwaka huu na linatarajiwa kuisha Oktoba mosi mwaka huu katika Ukumbi wa Sanaa Bagamoyo.





0 comments: