Social Icons

Tuesday, September 27, 2011

HARUSI YA NARGIS MOHAMED FULL SHANGWE!!!Nargis Mohamed Jiwa (kushoto), akilishana keki kwa staili ya siku hizi na mume wake mpendwa Idd Issa Suleiman Romore, katika Ukumbi wa Stallion Kawe Over kado jijini Dar es Salaam.
Keki ilichukua nafasi namna hii kwa wapendanao hawa.
Hapa Nargis na mumewe wakinyweshana 'Shampeni' mara baada ya kufunguliwa na kuombwa kufanya hiyo ikiwa kama ishara ya ufunguzi wa vinywaji ukumbini hapo.
Nargis na mmewe wakiteta jambo na mmoja wa wanakamati wa sherehe hiyo.
... akimsaidia 'kusevu' chakula mumewe.
Mama mzazi wa Bibi harusi Mrs Batuli Wogole, akichukua matunda tayari kwa msosi wa usiku huo.
Msanii wa Filamu Bongo Sintah (kulia), akiwa kwenye pozi na maharusi hao, anaemfuatia ni Mboni Masimba na rafiki yao wa kwanza kushoto.
Mmoja wa watoto waliokuwa wakimwaga maua katika sherehe hiyo akiwa katika pozi na mama yake muda wa msosi.
Sintah, akijiandalia mazingira ya kuweka sawa tumbo lake.
Mambo ya msosi yalikuwa hivi mahari hapo.
Waarikwa wakijinafasi kwa raha zao.
... full maraha usiku huo!!
Mambo kama haya... ilikuwa kawaida kutokana na raha zilizokuwepo ukumbini hapo.
Unaona mtu kati... na kibao cha Katumba!!!
Raha ya harusi kujimwaya mwaya Bhanaaa...!
Nargis ... hakutaka kuboa sherehe yake bhana .... kwahiyo hakuwa nyuma kuzungusha nyonga yake mahari hapo.
Mambo ya Cheers...
Bi harusi akicheza miondoko ya 'kwaito' na waarikwa.
Maharusi wakiwa katika pozi na watoto waliokuwa wakimwaga maua.
Wakati maharusi hao wakiingia ukumbini.
Sintah, Mboni na rafiki yao katika pozi.
Sintah, akiwa katika pozi na Jacqueline Patrick.
Sintah alijiachia namna hii kabla ya kuzama ukumbini hapo.
Salma Msangi (wa pili kulia), akitoka kupakuwa msosi.
Jack nae hakuwa nyuma kujiandalia msosi mahari hapo.
Waarikwa wakigonga msosi
Watu walipozi kwa utulivu kama inavyoonekana.
Mambo ya msosi

SHEREHE ya ndoa ya kihistoria ya Miss Tanzania namba tatu 2003/04, Nargis Mohamed Jiwa aliyofunga na mfanyakazi wa benki moja maarufu jijini Dar es Salaam, Idd Issa Suleiman Romore, imevunja rekodi kufuatia mambo makubwa yalijitokeza katika shughuli hiyo.

Sherehe hiyo iliyoshuhudiwa na MATEJA20, hatua kwa hatua ilichukua nafasi mwishoni mwa wiki iliyopita Septemba 24, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa The Stallion uliopo Kawe, Dar es Salaam ambapo ilihudhuriwa na waalikwa wa kada mbalimbali ndani na nje ya Bongo.

Kabla ya maharusi hao kutimba eneo hilo, wageni waalikwa walishuhudiwa wakiingia na magari ya kifahari ambapo kwa uchunguzi makini hakukuwa na mkweche hata mmoja wala teksi huku kila mtu akiwa amependeza ajabu.

Nargis ambaye pia ni staa wa muvi za Kibongo alizama ukumbini hapo akifuatana na mumewe Idd saa 2:45 usiku ambapo kiota hicho cha burudani kililipuka kwa shangwe na vigelegele kutoka kwa waalikwa na mashostito wake.

Baada ya mapokezi hayo, Nargis aliyekuwa akimeremeta kama nyota aliongozana na mumewe hadi meza kuu na ndipo ratiba ya shughuli hiyo ikaanza kufuatwa rasmi.

Shughuli hiyo ilianza kwa wanandoa hao wapya kufungua ‘shampeni’ kisha wakakata keki na kutumia muda wa kulishana keki kufanya utambulisho wa wageni wa pande zote mbili huku vinywaji vya bei mbaya vikiendelea.

Kabla ya kujisogeza kwenye meza ya maakuli, wanandoa hao waliburudisha kwa muziki kidogo kisha wakarejea meza kuu kuendelea na ratiba ya shughuli hiyo.

Baada ya utambulisho na muziki kidogo, muda wa msosi uliwadia ambapo wanandoa waliwaongoza waalikwa hadi meza ya chakula.

Watu waligonga maakuli ya maana yaliyosheheshwa na nyama za kumwaga za kupikwa, kuaangwa na kuchoma.

Muda mwingi Nargis aliyeuza nyago kwenye Filamu ya Yellow Banana alionekana kuchangamka kupita maelezo na ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuonekana ‘beneti’ na mumewe huyo.

Mastaa wa Kibongo waliohudhuria waliongeza utamu kwa namna walivyopendeza na kuifanya sherehe hiyo kuonekana ya kifahari.

Baadhi ya mastaa hao ni pamoja na muigizaji Christina Manongi ‘Sintah’ modo Jacqueline Patrick, watangazaji Salima Msangi, Sakina Lyoka na Miss Mbeya wa miaka ya nyuma, Mboni Masimba.

Baada ya zawadi na shughuli zote huku maharusi wakizunguka kila meza kuwapa waalikwa mkono wa heri, walifungua muziki wa kufa mtu na kuserebuka muziki wa maadhi ya Kwaito.





3 comments:

Anonymous said...

Mkuu ushauri wa bure sio waarikwa ni waalikwa. jamani wanahabari lugha muhimu katika blog zenu. pls
usibanie kwa faida yako na wanahabari wenzako.

Anonymous said...

jamaan acheni kucopy na kupaste..yaan hayo maneno baada ya picha naona blog sijui ngapi zimeandika same thing...be creative.

Anonymous said...

duuh