Social Icons

Wednesday, November 30, 2011

JERRY MURO AACHIWA HURU

Jerry (kushoto) akiingia na wakili wa utetezi, Majura Magafu.

...Akisindikizwa na mkewe, Jennifer John, kuingia chumba cha hukumu.
MTANGAZAJI maarufu wa televisheni na radio nchini, Jerry Murro, aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kupokea rushwa, leo ameachiwa huru na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Frank Moshi, baada ya mahakama hiyo kubaini mapungufu yalikuwemo upande wa mashitaka kwenye mwenendo mzima wa kesi hiyo. Akikubaliana na hoja za upande wa utetezi, aliwaachilia huru pia wenzake wawili ambao ni Edmund Kapama na Deogratius Mgasa.


Mshitakiwa namba tatu katika kesi hiyo, Edmund Kapama, akielekea chumba cha hukumu.

Jerry akitoka na mkewe kwa furaha baada ya kuachiwa huru.
…Akionyesha ishara ya dole baada ya kuachiwa huru.
…Akiongea na wanahabari baada ya kuachiwa huru.
Mapaparazi wakimzingira (Jerry) kumpa pole na kumhoji.

Jerry akiondoka mahakamani na mkewe.



TIGO KUFUNGA MWAKA NA PROMOSHENI YA 'ZAMU YAKO KUSHINDA'

Afisa Viwango wa Tigo, Pamela Shellukindo (kulia), akifafanua juu ya shindano hilo, na mfanyakazi mwenzake wa idara hiyo Benedict Mponzi.

Benedict Mponzi akijibu moja ya maswali kutoka kwa waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo.

Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwajibika kwenye kikao hicho.
KAMPUNI YA mawasiliano ya simu za mkononi Tanzania, Tigo, leo, Novemba 30, imetangaza shindano lenye ujumbe wa ‘Zamu Yako Kushinda’ itayoendeshwa ndani ya siku 82 ambapo mshindi wa kwanza atazawadiwa 4,000,000.

Haya yalielezwa na maofisa wa Tigo, Pamela Shellukindo na Benedict Mponzi katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Kwa mujjibu wa maofisa hao, mshindi wa pili atajinyakulia kompyuta aina ya ‘Laptop’ mpya kutoka kampuni ya Samsung.
Tigo imeamua kuanzisha shindano hilo ili kuwapa changamoto wateja wake na kutoa nafasi za kushindi kwa wale wa malipo ya kabla na ya baadaye ambao walishiriki katika shindano lililopita.

Washiriki wanatakiwa kutuma ujumbe mfupi kuanzia saa sita kamili usiku wa tarehe 30/11/2011 mpaka saa 11: 59 usiku wa tarehe 19/12/2012.

Ili kushiriki, unatakiwa kutuma neno ‘Tigo’ kwenda namba 15571, kila meseji itagharimu kiasi cha shilingi 450, na wanaotakiwa kushiriki ni wale wote wenye umri wa miaka 18 tu.




CHAMA CHA WAAJIRI (ATE) KUHAMASISHA UPIMAJI UKIMWI DESEMBA MOSI

Mwenyekiti wa ATE, Cornelius Kariwa (kulia), akifafanua namna utaratibu huo wa upimaji utakavyokuwa. Kushoto ni Mkurugenzi wa chama hicho, Justina Lyela.

Wanahabari wakichukua matukio muhimu katika mkutano huo.

Sunday, November 27, 2011

CHADEMA WAKUTANA NA RAIS KIKWETE IKULU

Baadhi ya viongozi wa Chadema wakiingia Ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni.

Mhe. Rais Kiketwe akisalimiana na Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mboe mara baada ya kuingia Ikulu.

Mhe. William Lukuvi akisalimiana na Mhe. Tundu Lissu.

Mhe. Mbowe akiongea na Mhe. Rais.

...safu ya viongozi wa Chadema ikiongea na Rais.

Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chadema mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu mapema leo.



FABOLOUS, INTER COLLEGE YAPAGAWISHA MASHABIKI DAR

Fabolous akifanya makamuzi.


..Sehemu ya nyomi iliyohudhuria


Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi.

SHOO ya Inter College Bash iliyokuwa inahusisha vichwa makini kutoka nchini Marekani na hapa Bongo, usiku wa kuamkia leo ilifana vilivyo katika viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam, ambapo Fabolous aliweza kupiga shoo iliyochukua zaidi ya dakika 30 wakati wazawa wakitumia zaidi ya saa nane. Mbali na Fabolous ambaye ilikuwa kawaida kwake kufanya vizuri, wasanii wa Bongo waliosisimua mioyo ya mashabiki wao ni Juma Kassim ‘Juma Nature’ na kundi zima la Wanaume Halisi, Seleman Msindi ‘Afande Sele’, Wanaume Family, Haroun Kahena ‘Inspector Haroun’ akiongoza kundi zima la Gangwe Mob. Wengine ni Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’, Jay More, Nako 2 Nako, Joe Makini , Niki wa Pili, Elias Barnaba, Manzese Crew, Kikosi cha Mizinga kikiongozwa na Kala Pina na THT Dances.


Selemani Msindi 'Afande Sele' akiwa kazini.


Kiongozi wa kundi la Gangwe Mob Haroun Kahena ‘Inspector Haroon’ (kushoto), akionyesha uwezo wa kundi hilo na mwenzake Luteni Kalama.


Naseeb Abdul ‘Diamond’ akiwajibika.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo ‘Hamisi Mwijuma ‘Mwana FA’ (kulia), akitoa burudani na msanii mwenzake, Shetta.


Joe Makini naye hakuwa nyuma kutoa burudani.



VINEGA WAPAGAWISHA USTAWI

Wasanii wa kizazi kipya waliowahi kutamba zamani waliounda kundi la Vinega wakiongozwa na Mkurugenzi wa Deiwaka Entertainment, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (pichani juu) usiku wa kuamkia leo wamefanya onesho lililohudhuriwa na maelfu ya watu katika Viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam. Yafuatayo ni baadhi ya matukio yaliyojiri kiwanjani hapo:.

...sehemu ya yomi iliyokuwepo

Mwekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Freeman Mbowe, akiwapa hai, mashabiki kabla ya kuanza kuchana mistari.

Sister P akikamua.

...Zay B jukwaani

..Daz baba na makamuzi yake

Dj Sox wa Mabaga Fresh

Mkoloni akiwajibika

Mkoloni akiwajibika

Mr. Simple, ambaye pia ni Diwani kwa tiketi ya Chadema

...Kinadada wakifuatilia makamuzi

...Mashabiki wakiwa na mzuka

...Sugu anapoweka pembeni uheshimiwa na kukamata Mic


Dada wa kitasha akiserebuka baada ya kunogewa na bongo flava



TAMASHA LA STREET UNIVERSITY LARINDIMA ARUSHA

..Tamasha la Street University linaendelea hivi sasa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha na pichani ni sehemu ya umati uliyopo uwanjani hapo hadi sasa.

....baadhi ya wasanii wa Glorious Singers wakiwa jukwaani wakitumbuiza

...mmoja wa wahamasishaji wa Street University, James Mwang'amba, akifuatilia semina ya Ujasiriamali katika ukumbi wa Corridor Spring Hotel jana

...Eric Shigongo akitoa darasa la ndani la Ujasiriamali ndani ya hotel ya Corridor Spring Hotel jana jijini Arusha



Thursday, November 24, 2011

JINI KABULA ATIMULIWA KWA ‘BWANA’KE’


Na Brighton Masalu

NYANGUMI anaye

piga mbizi katika bahari ya filamu za kibongo asiyeishiwa na vimbwanga kila jogoo wanapouaga usiku mmoja, Miriam Nyafulwa Jolwa ‘Jini Kabula’ juzikati alionja chungu ya maisha baada ya kupewa ‘Red card’ nyumbani kwa anayedaiwa ni ‘bwana’ake’ anaye tambulika mjini kwa nomino ya Waukweli, Mateja20 imebugia ushahidi wa kutosha.

Kikianika mwanya mbele ya balozi wa mateja20, chanzo makini cha habari hii ambacho ni rafiki mkubwa wa mkurya huyo, hivi karibuni kilitambaa na sentensi kuwa , Waukweli amemtimulia mbali Kabula baada ya kumhisi anatoka kimapenzi na mdogo wake aliyemtaja kwa jina la Nchumi.

Kikulacho hicho kiliendelea kuachia paragraph moja baada ya nyingine kwamba maisha ya Kabula na Nchumi kwa sasa yamehamia Makumbusho Kijitonyama kwa rafiki yao ambaye anaelea mjini kwa nembo ya U-miss Ruvuma mwaka 2008 -09, Isabella Mpanda.

“Pamoja na kuhamishia kambi huko Waukweli amekuwa akiwawinda kila kukicha ambapo juzikati aliwakuta Kinondoni wasaga lami katika matembezi ya hapo na pale na kujikuta akimpola simu Nchumi, ambapo Kabula aliingilia, na kusababisha eneo hilo kugeuka ‘Libya’ kwa ugomvi mkubwa lakini mwisho wa siku Waukweli alitokomea kitaa na ‘kilongalonga’ hicho” kilihabarisha chanzo chetu na kuongeza:

“Walimuacha X yuho wa Mr. Chuzi na Nchumi wakilalama huku wakiahidi kufuatilia simu yao na asipo itowa watahakikisha nao wanamlia patro ili kumfuanyia kitu ambacho hatakuja kukisahau katika life yake yote,” kilifunika lips .

Mateja20, baada ya kuzinyaka ‘Nyiuzi’ hizo ilipereruka angani katika jiji la Meck Sadick kikiwasaka wahusika ili kujua yapi ni maziwa na lipi ni tui la nazi juu ya udakaua huo ambapo Jini na mwenzake walikiri kupewa ‘go ahead’ na dumejike huyo kutoka nyumbani kwake, lakini cha ajabu ni kwamba bado ana wafanyia ‘Ugadafi’ bila hatia.

“Nashangaa kwake tumemtokea lakini haishi kututafuta sijui anataka tumfanyie nini ili alizishwe na maisha haya maana yeye yuko na mkewe … sasa sijui bado anahitaji nini kwetu maana aliona sisi hatufai tena kuishi nae na tukamtokea sisi hata hatumueliwi kabisa,” alibainisha Jini Kabula huku akikimbiza macho pembeni mwa kamera ya Mateja20.