Social Icons

Saturday, May 22, 2010

STONE MAYIYASIKA HAWAVUMI LAKINI WAPO!


: Baadhi ya safuu ya waimbaji wa Stone Mayiyasika wakiongozwa na Maru Stonchi wa kwanza kushoto wakishambulia jukwaa namna hii.

: Nafikiri kuacha mambo nje ni moja ya ka’sitaili kao bwana!

Duuh! Kumbe kibur… kikio nje bora nifunike kwa mkono sasa!

Mnenguaji wa bendi hiyo akifanya makamzi huku akiwa ameacha mambo nje!

DIAMOND MUSIC KILA IJUMAA MEEDA!

Bendi ya muziki wa Dansi nchini Diamond Music itakuwa ikitoa burudani kila siku ya Ijumaa ndani ya Ukumbi wa Meeda Club uliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.

Akitoa habari hii kwa msisitizo zaidi mkurugenzi mtendaji wa bendi hiyo Judis Moshi alisema kwamba tayari ameshakamilisha mazungumzo na uongozi wa Meeda kinachafuatia ni wao kuhakikisha wanaburudisha mashabiki wao kila siku ya Ijumaa.

Judis ametumia fursa hiyo kuwaomba mashabiki wake wote wajitokeze kwa wingi ili kutoa sapoti ya kutosha kwa bendi hiyo.

Rais wa Bendi ya Diamond Music Mulemle katikati akiongoza makamzi ya hatali na waimbaji wenzake ndani ya ukumbi wa Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo.

Friday, May 21, 2010

TUNDAMAN NA MADEE KWENYE MIPASHO HAWAJAMBOOOOOO…


Wasanii wa ubongo wa fleva nao hawakuwa nyuma kwani walipanda stejini kuwasalimu mashabiki wa bendi hizo. Kushoto ni Tundaman na Madee (kulia).

MZEE WA PAMBA ATAMANI JUKWAA!


Mfanyabiashara alwatani wa vimini vya wanawake ndani ya soko la Makumbusho, Pius Rutta ‘Mzee wa Pamba’ alikuwa akitamani kuvamia jukwaa kwa midadi iliyokuwa imempanda.

HAPO CHACHA…


Mashabiki wa bendi hizo walijiachia kwa raha zao.

DIDA AWA MR PAPARAZI!!!!


Mtangazaji wa kipindi cha Mirindimo ya Pwani kunako Radio Times FM, Khadija Shahibu ‘Dida’ aligeuka Mr Paparazi katika shoo hiyo.

FM ACADEMIA, JAHAZI WAFUNIKA



Bendi za FM Academia na Jahaz Modern Taarab usiku wa kuamkia leo walifunika mbaya ndani ya Mango Garden, Kino, jijini Dar.

CHOKI AKIKABIDHIWA MILIONI TANO


Choki akibidhiwa kitita cha milioni tano kutokwa mkurugenzi wa Abama Inc, Eddy Magoma (kushoto).

ALLY CHOKI KUTAMBULISHA RASMI EXTRA BONGO MEI 28


Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo ‘Mjini Mipango’ Ally Choki ‘Mzee wa Farasi’ anatarajia kuitambulisha rasmi bendi yake wiki ijayo Mei 28, mwaka huu pale Msasani Club Kinondoni, jijini Dar.
Akiongea na Mateja 20 ndani ya Triz Motel Mbezi Beach jijini Dar jana ambapo alikabidhiwa kitita cha milioni 5 kutoka kwa wadhamini wakuu wa utambulisho huo, Abama Inc, jamaa alisema ishu hiyo itakuwa ya kihistoria kwani mwanamuziki Adolf Domingeze kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) atafanya kweli.

Wasanii wengine wa Bongo watakaopoteza ile mbaya ni pamoja na Matonya, Husein Machozi, Prof Jay na wengine. Siyo shoo ya kukosa watu wangu!

MASELE CHAPOMBE: DEMU WANGU ANA ‘INYE’ ILA SIYO LA KICHINA!


Mambo vipi wakubwa kwa wadogo? Ni matumaini yangu kuwa mko poa sana na hapa tunaendeleza libeneke lile lile, yaani burudani.
Baada ya wiki iliyopita kuwa na mmoja wa mapresenta wa program ya Leo Tena kunako Redio ya Watu, Cloud FM, Zamaradi Mketema, wiki hii tunamleta kwenu ‘Komediani’ wa Kundi la Mizengwe linalovunja mawingu kupitia Kituo cha Runinga cha ITV, Crispine Masele ‘Masele Chapombe’.

Masele ni mzaliwa wa Shinyanga, lakini alikulia pande za Iringa na Dar kufuatia hamahama ya wazazi iliyokuwa ikisababishwa na kazi. Kwa sasa Masele anaishi pande za Mikocheni A, jijini Dar akipiga mzigo wa kurekodi filamu za vichekesho. Mbali na kazi hiyo, pia jamaa ni mfanyabiashara wa mitumba katika sehemu mbalimbali za Jiji la Dar. Ili kupata kitu kamili ungana naye akijibu sindano kumi za moto za safu hii.

TQ: Unaweza kukumbuka ni lini ulianza kufanya kazi za usanii na ni nini kilichokuvutia hadi ukajiingiza huko?

MASELE: Kazi ya sanaa niliianza mwaka 2005 nilipoamua kujiunga katika Kikundi cha Dar Talent kilichokuwa na maskani yake jijini Dar es Salaam. Sanaa hiyo nilikuwa nayo moyoni toka siku nyingi kwani nilikuwa nikijiona mwenye kipaji hicho tangu kitambo.

TQ: Kwanini uliamua kutumia stahili ya kuwa mlevi hadi ukapachikwa jina la Masele Chapombe?

MASELE: Nilipokuwa Dar Talent, mwalimu wangu alinitaka kuonesha kipaji changu cha uchekeshaji. Nakumbuka iliniwia vigumu kwani wasanii wenzangu walikuwa wako juu zaidi kuliko mimi, hivyo siku hiyo nilikosa kitu cha kuigiza kwani sikupenda wote tufanane kwa kuigiza vitu vinavyofanana.

TQ: Kwa hiyo ilikuwaje hadi ukaamua kutumia staili hiyo?

MASELE: Siku hiyo niliporudi nyumbani nilikutana na a jirani yangu ambaye alikuwa amelewa akiwa anazungumza maneno mengi na kufanya mambo mengi ya kuchekesha, lakini pombe ilipokatika, alipoulizwa alishindwa kukumbuka vituko vyote alivyokuwa akivifanya.

TQ: Masele kuna tetesi kwamba una tabia ya kulewa kiukweli. Je, ni kweli?

MASELE: Licha ya kutokuwa mlevi kama wengi wanavyodhani, nimetumia kipaji changu kuigiza hadi sura ya mtu mlevi inavyotakiwa kuwa pamoja na mwili wake na vituko vya walevi, jambo ambalo huwa linawashinda wasanii wengi nchini kwa kuwa wanakosa uhalisia.

TQ: Nini mafanikio yako katika kazi ya sanaa?

MASELE: Mbali na kutambulika, lakini biashara zangu zimekuwa zinakwenda mwake mwake. Sanaa inaniweka mjini chini ya Meneja wangu, John Dickson. Filamu zangu kama Inye Plus, Inye Mbwetembwete na nyingine kibao, zinanifanya niwake mjini.

TQ: Mbali na mafanikio hayo lakini baadhi ya wasanii wakipata chochote kitu hukimbilia kununua vitu vya starehe kama magari na matanuzi mengine. Je, kwako wewe hili likoje?

MASELE: Ni kweli ‘but’ kwa upande wangu niko kwenye maandalizi naangusha bonge la mjengo pande za Mbezi Shamba, jijini Dar.

TQ: Katika kila kazi kuna vigingi na Vikwazo. Je, kwa upande wako hali ikoje?

MASELE: Binadamu na mashabiki wangu wajue kuwa ulevi siyo sababu ya kudharauliwa mtaani au katika jamii. Mara nyingi naambiwa nimelewa wakati mimi niko safi, unakuta hata sijalewa.

TQ: (Swali la kifuta jasho) Masele umeoa?

MASELE: Sijaoa, lakini nina mke mwenye makalio makubwa ‘Inye’ ambaye ni raia wa Italia, mtu na shughuli zake.

TQ: Umesema ana makalio babkubwa, Je, ni ya Kichina?

MASELE: Kile ni kitu orijino, siyo cha Kichina.

TQ: Ni nini matarajio yako ya baadaye na unawaambia nini mashabiki wako?

MASELE: “Natarajia kufanya makubwa katika fani ya vichekesho na filamu kwa ujumla. Mashabiki wangu walikuwa wakinidai filamu yangu, nimefanikiwa kuwapatia filamu hiyo nikiwa nikiwa na wasanii chipukizi sasa nitarudi kuendelea na Mizengwe kama kawaida," anasema Masele Chapombe.

KIMWANA WA MAISHA PLUS



Aliyekuwa mshiriki wa maisha Plus 2010 Jacqueline Dastan akiwa katika picha ya pozi.

ETI! HII SAWA KWA MASHOSTITO?


Kimwana Manywere namba mbili 2006/07 Husna Idd ‘Sajenti’ walipatikana wakirishana keki kwa mdomo na shostito kipenzi wake Baby ilikuwa siku ya Birthday ya Baby iliyofuanyika maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

KALALA NA MY WIFE WAKE!


Mwanamuzi matawi ya juu wa Bendi ya The African Stars International ‘Twanga Pepeta Sugu Kisima Cha Burudani a.k.a Wazee wa Kisigino’ Kalala Junior kwa mara ya kwanza anapatikana katika picha ya pozi la mahaba na kiburudisho chake cha moyo Mary Junior katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni jiji Dar.

TINGISHA HATA KUSA TENA JUKWAA!


Mnenguaji tegemezi wa Bendi ya Diamond Music Khadija Tingisha anadaiwa kutopanda tena stejini kutokana na ujauzito wake kumuelemea habari kutoka ndani ya bendi hiyo zinasema wameamua kumpumzisha kwa muda kukata mauno kutokana na ushauri wa kiafya kutoka kwa Madaktari.

WEMA HAWATUWEZI…..


Mrs Chalz Baba Wema akionyesha staili ya hamuwezi kumfanya lolote wala kusikia kwa Charlz Baba! Siku chache alipo wasili katika kiwanja cha ndege cha Taifa cha Mwalimu Julius K Nyerere jijini Dar es Salaam akitokea Malaysia kuchukua vyeti vyake.

CHALZ BABA,WEMA NATAKUWA NA WEWE MILELE!


Mwana dare es Salaam Charlz Baba walinaswa wakiwa wamekumbatiana na My wife wake Wema Septu katika kiwanja cha ndege cha taifa cha Mwalimu Julius K Nyerere jijini Dar es Salaam.

CHAPOMBE HAKIKA TUNAWAKIRISHA!


Msanii wa Komedi katika kundi la Mizengwe maarufu Masele Chapombe akiwa kwenye picha ya pozi katika Viwanja vya Leaders Club Kino, jijini Dar es Salaam.

HAFISA KAZINJA KAPATIKANA DAR?


Mwanamuziki wa miondoko ya Bongo fleva Hafisa Kazinja hivi karibuni alipatikana akishuka ngazi katika jengo la Biashara Complex baada ya kuadimika mjini kwa muda mrefu, hapa anashuka ngazi akitokea ofisi za Bendi ya Akudo Impact zilizopo katika jingo hilo Mwanayamala Komakoma jijini Dar es Salaam.

MARAFIKI WA KWELI TWANGA!





Warembo wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ Sabrina Mbetembete (kushoto)akiwa kwenye picha ya pamoja na shositito Asha Said ‘Shalapova’ katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.

KUBADIRISHANA MATE SI ISHUU KWAO!!!















Wema akilambana mdomo na kakiburudisho kake Chalz Baba hivi juzikati maeneo ya Ilala jijini Dar

JOSE MARA AKAMILISHA CHOZI LA YATIMA

Mwanamuzi nyota wa FM Academia ‘Wazee wa ngwasuma’ Joseph Michael ‘Jose Mara’ hatimaye amekamilisha albam yake mpya inayokwenda kwa jina la Chozi la Yatima.
Akiongea na muandaaji wa mtandao huu juzikati Jose Mara alisema kwamba albam yake iliyotayali inazaidi ya nyimbo kumi na mbili na kwamba iko katika mahadhi tofauti tofauti akiwa na maana ya kwa kila sitaili inapatikana katika albam hiyo ambayo anatarajia kuitupa kitaani hivi karibuni.

Jose mara akiajibika kwa juhudi zote jukwaani jana katika ukumbi wa Mango Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo bendi yake ya FM Academia ilikuwa ikigandamiza burudani pande hizo

Thursday, May 20, 2010

KUBADIRISHANA MATE SI ISHUU KWAO!!!


Wema akilambana mdomo na kakiburudisho kake Chalz Baba hivi juzikati maeneo ya Ilala jijini Dar.

MAMBO YA MAHABA MAZITO!


Miss Tanzania 2006/07 Wema Septu (kushoto) akimshika shavuni kwa mapozi Chalz Baba hivi karibuni maeneo ya Afre center Ilala jijini Dar es Salaam.

MKURUGEZI KATIKA POZI


Mkurugenzi mkuu wa Zizzou Fashion Tippo Athuman (kulia) akiwa kwenye picha ya pozi na Godwin Gondwe ‘Double G’ mtangazaji wa Redio One na ITV ndani ya Atriums hoteli Sinza siku ya Dinner Part.

NYANDU TOZI STEVE HAWAKUWA NYUMA KUUNDA POZI!!


Mkali wa miondoko ya R&B Steve (kulia) akiwa kwenye pozi la hatari na Hamidu Salim ‘Nyandu Tozi’ndani ya Atriums hotel Sinza afrikasana jijini Dar es Salaam.

SIYO ISSUE KUNG’ARISHA MDOMO!!


Light na Angel wakiwa katika pozi la pamoja siku hiyo ya Dinner Part iliyoandariwa na Zizzou Entertainment ndani ya Atriums hotel.

KWENYE POZI ZAIDI WAKO HIVI!!!


Wa kwanza kushoto ni Angel akiwa kwenye picha ya pozi na wafanyakazi wenzake Light (katikati) na kulia ni Waiya a.k.a Manka kwenye Dinner Part Atriums hotel

DU! KAMA HANA HABARI VILE!


Mfanyakazi Mkongwe wa Zizzou Fashion Maarufu kwa Waiya a.k.a Manka naye alikuwepo Atriums hotel.

NYANDU TOZI HAKUWA NYUMA!


Brother Man Hamidu Salim a.k.a Nyandu Tozi alikuwepo katika kukamirisha mpango mzima wa makuli ya usiku yaliyokuwa yameandaliwa na Zizou Entertainment ndani ya Hotel ya Atriums Sinza Afrika sana.

DAH! KUMBE MAMBO YANAKUAGA HIVI?


Shositito huyu anakwenda kwa jina la Angel ni mmoja wa wafanyakazi wa Zizou Fashion akifuatilia kwa makini mpango mzima wa Dinner Part hiyo.

NIMUONEKANO WAKE TU KATIKA POZI!!


Mrembo anayekwenda kwa jina la Glory hilo ndilo jina maarufu, anapiga mzigo ndani ya nduka la Zizzou Fashion Sinza Afrika sana na hapa ilikuwa siku ya Dinner Part ndani ya Hotel ya The Atriums iliyopo maeneo ya Sinza Afrika Sana karibu na duka analofanyia kazi.

Tuesday, May 18, 2010

DAH!! NIKWELI PETTY MAN ULIMISI WEMA!!!


Brotherman toka pande za kino Petty man a.k.a mdogo wa Chalz Baba,aki hug kwa furaha na shemeji yake Wema Sepetu

HUYU NDIYE SHAMSA BWANA!!


Mrembo ndani ya film industry Shamsa Ford akiwa kwenye pozi lakipekee katika sherehe ya kutimiza
Miaka ishirini na nne Kyalaa Seheye iliyofanyika Sinza kumekucha nyumbani kwa Aunty Ezekiel hivi juzi kati.

SHOW YA MWISHO YA SUZI KABLA HAJA NG’OKA TWANGA!


Mnenguaji wa bendi ya African Stars Twanga pepeta Suzani Chugwa ‘Queen Suzy’ siku alipo bambwa akiwa ameninginia juu ya nguzao ya jukwa la Mango Garden siku chache kabla yakusepa Umangani

ASHA BARAKA GOMBEA UBUNGE URAMBE KURA ZETU!


Baadhi ya Wadau wa Kampuni ya ‘ASET’ Hapa wanaonekana wakiwa wameshikilia kadi za kupigia kura huku wakimsisidizia Asha Baraka agombee Ubunge ili wapate kupingia kura katika uchaguzi mkuu ujao. Vijana hawa walionekana wakimuonyeshea vitamburisho vyao katika Viwanja vya Leaders Club kinondoni Dar hivi karibuni.

MBONA MMEKUWA ADIMU TWANGA?


Wanenguaji miaka kitambo ndani ya Bendi ya Twanga Pepeta (Majina kapuni) hivi karibuni wadau wa mambo ya kudansi wamekuwa wakiulizia marakwamara upotevu wa wakata nyonga hawa ambao wanataklibani miezi mitano hawaonekani Kwenye game na kwamba hawajurikani ni wapi walipo je, kwa staili hii wanaweza kulejea?

CHOKORAA, THEA NI YEYE YULE YULE!


Rapa Big name FROM The African Stars International ‘Twanga Pepeta Sugu kisima cha Burudani’ Khared Chuma ‘Chokraa’ Hii inaenda sambamba na vesi zake alizovunja katika song ya ‘Siri ya mapenzi’ kwani nasema hivi nikiwa na maana sawa kwamba siku chache tu baada ya kuonekana kila kona wakiwa closed na Thea Desminder Girl a.k.a kiburudisho cha Chokoraa hivi juzi kati wameonyesha kutemana kwa mabango makubwa hari inayoashilia kutolejeana tena mabango hayo wamekuwa wakishikiana mabango kila mara hasa pale anapotokea mtu na kuulizia juu ya uhusiano wao. Ishu hizo zimekuwa zikitawala ndani ya kumbi mbalimbali za burudani.

TINNO NA GRACE YA MVINYO!


Msanii wa Filam Bongo Hissan Muya ‘Tinno’ Kama kawaida yake huwa hatii uzembe wala kurudi nyuma hasa anapokuwa katika sherehe katika suala zima la kutafuna bata mkononi mwake kashikilia Grace me naona kama soda hivi! Lakini kwa upande wake anasema duh! bro’ sikamatilii mkononi mwangu grace bila mvinyo! Ebwana hii ni staili yake kama vipi muacheni aburudike ki mpango wake.

BILA SHAKA HUYU ATAKUWA NI MHUSIKA!


Bila shaka hapa nitakuwa namzungumzia Nasoro Awardhi ‘Cheki Budi’ nakama sikosei itakuwa wazi kabisa hapa amekaa sambamba na the kiburudisho chake japokuwa ukimuuliza harakaharaka kubisha ni suala la kufikia, kwa mujibu wa blog hii inathubutu kuwaweka wazi kwa staili hii ya mkaa wao ambao walikutwa Ndani ya kiwanja cha Makete.

MZEE CHILO SAMBAMBA NA KIBURUDISHO CHA NANII!


Mcheza filamu matawi ya juu na mwenye sifa lukuki za kuvaa husika katika Vipande anachopangiwa anapokuwa katika suala zima la uigizaji Ahamed Olotu ‘Mzee Chilo’ siku moja katika pitapita za muandaji wa blog alifanikiwa kuinasa picha hii akiwa ameuchubua sti moja na Kiburudisho cha mwanafilam mzwenzake kama hakifahamu vile, iwapo mpango wote huu ulikuwa ndani ya Kumbi wa Makete Mbezi beach jijini Dar.

HII NI SAWA DOKTA CHENI!


The big name from film Industry Muhsini Awadhi ‘Dokita Cheni’hivi juzi kati alinaswa na Kamera yetu akiwa ameuchubua kiaina na my wife wake misili ya bubu. Ishu hiyo ilinaswa ndani ya Ukumbi wa Makete katika pati ya celebrity mwenzake Emmanuel Myamba Mbezi beach jijini Dar.

MAMBO YA KANGA TUPU NA NEWS PAPER


Mrembo ana kwenda kwa jina la Moshi anatokea pande za Rock City Mwanza maisha yake zaidi ni ndani ya jiji la Lukuvi anapoa pande za Sinza Moli hapa alinaswa akiwa Kwenye kanga tupu huku akijiburudisha na news paper ki mtindo.

HAPA VIPI WADAU ANAWEZA HAWEZI?


Mrembo mpya ambaye tayali ameshashika kasi kubwa ndani ya tasnia ya Filam nchini anakwenda kwa jina la Shamsa Ford hapa yuko katika pozi la mahaba je, utahoji namba yake kweli au utaipenda?

NI MIPANGILIO TU CHOCHOTE KINAWEZEKANA!


Beatify the Big name & Big Body kutoka ndani ya Maisha Plus Efrancyia akiwa Kwenye picha ya pozi zito.

Wednesday, May 5, 2010

HAPA VIPI AUNT NA POZI LA MAHABA!


Mkali kutoka ndani ya Film Industry Aunt Ezekiel hivi juzi kati alibambwa na kamera yetu akiwa katika picha ya pozi la mahaba mazito ukiiangalia sana hukawii kutafuta namba yake!