Social Icons

Thursday, September 30, 2010

MOHAMMED MWIKONGI ‘FRANK’: Sijawahi kutumia jina langu kung’olea mademu!

NAJUA mtakuwa mmeimisi sana safu yenu hii ambayo hukuletea mastaa mbalimbali wa Bongo ambao hugusia masuala mbalimbali yahusuyo maisha yao kupitia maswali kumi ambayo huwa nawauliza. Nilikuwa nimebanwa kidogo lakini sasa nimerejea.
Wiki hii namleta kwenu msanii anayefanya vizuri kupitia kiwanda cha filamu Bongo, Mohammed Mwikongi ‘Frank’. Kabla ya kwenda kwenye maswali niliyombana nayo kwanza tupate historia yake kwa ufupi.
Mshikaji alizaliwa miaka 31 iliyopita katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam na mwaka 1987 alijiunga katika shule ya msingi Mapambano na kuhitimu mwaka 1993. Frank alikuwa ‘kichwa’ flani kwani alifaulu na kujiunga kidato cha kwanza katika shule ya Highlands Secondary School iliyopo mkoani Iringa na kuhitimu mwaka 1997. Mwaka 1998 alijiunga katika Sekondari ya Jitegemee jijini Dar es Salaam na kumaliza kidato cha sita kisha kujiunga na chuo cha habari cha DSJ ambapo alichukua Diploma ya Habari.
TQ: Dah! Kumbe wewe ni msomi? Enhee baada ya kuhitimu masomo yako ya uandishi wa habari, ilikuwaje sasa ukajikita katika masuala ya uigizaji wa filamu badala ya kuitumia taaluma yako?
Frank: Uigizaji ulikuwa katika damu yangu, niliipenda fani hii tangu nilipokuwa mdogo ndiyo maana hata nilipohitimu DSJ haikuwa kitu cha ajabu mimi kujiingiza kwenye uigizaji.
TQ:Unavyo vyeti vya uandishi wa habari, ulishwahi kufanya kazi sehemu yoyote kama mwandishi, mtangazaji au afisa uhusiano?
Frank: Nilishawahi kufanya kazi katika kituo cha Star TV kama ripota baada ya kuhitimu masomo yangu na baada ya hapo nilipata shavu Benchmark Production katika kipindi cha Wimbo.
TQ: Hivi unadhani filamu inalipa zaidi kuliko uandishi kiasi cha kuamua kuipa kisogo taaluma yako?
Frank: Awali nilibaini kwamba, nina ‘wake’ wawili yaani huku ni muandishi lakini pia ni muigizaji, hivyo nikaona siwezi kutumikia wake wawili kwa wakati mmoja,nikaona kwa kuwa naiweza vizuri sanaa bora niitumie hiyo katika kuyaendesha maisha yangu.
TQ:Unaweza kuimbuka filamu yako ya kwanza kuicheza na ikaingia mtaani? Ilipotoka ulijisikiaje?
Frank: Filamu yagu ya kwanza naikumbuka vizuri, ilikuwa inaitwa Chumba Namba 77. Filamu hii iliandaliwa na Christian Mhenga. Kusema kweli ilipotoka nilisikia furaha ya aina yake ambayo siwezi kuielezea kwa maneno.
TQ:Turudi kwenye maisha yako ya kimapenzi, umeoa wewe au bado uko singo?
Frank: Nimeoa ila kwa sasa siwezi kumzungumzia mke wangu kwa undani.
TQ:Vipi watoto, umejaaliwa kuwa nao?
Frank: Ninao watoto wawili ambao ni Tariq na Sharline, nawapenda sana wanangu.
TQ:Huko nyuma ulikuwa na urafiki wa karibu sana na viraka wa filamu nchini, Steven Kanumba na Vincent Kigosi ‘Ray’ lakini sasa hivi inadaiwa hampikwi chungu kimoja, habari hizi zina ukweli ndani yake?
Frank: In short, Ray na Kanumba ni wadogo zangu, nilibaini pia umri walionao huenda ulikua ukichangia katika yale waliyokuwa wanayafanya hivyo nikaamua kujiepusha nao, hata hivyo tulikaa tukasuluhishwa ingawa mapungufu huwa hayakosekani lakini kwasasa hamna shari.TQ: Imekuwa ikitokea sana kwamba, wasanii wenye rika kama lako kutafunwa na skendo za ngono zembe huku wakihusishwa na wasanii wao wa kike, kwako hili limekaaje?
Frank:Kwa upande wangu suala zima la ngono zembe huwa silipi nafasi na wala sijawahi kutumia jina langu kuchukulia mademu. Pamoja na hilo sikatai kama hakuna wenye tabia hiyo ila mara nyingi wenye tabia hiyo huwa hawadumu katika fani.
TQ: Ni akina nani hasa ndani ya sanaa ya uigizaji ambao hawaitendei haki fani?
Frank:Kaazi kweli kweli! Ok wasanii wa aina hiyo wapo tena wanafahamika na wengi wao ni maproducer. Mara nyingi huwa naona bora waachane na sanaa wachukue majembe wakalime kwani wanakoipeleka sanaa siko kabisa.
TQ:Ni mafanikio gani ambayo umeyapata tangu umeamua kujiingiza katika fani hii ya uigizaji?
Frank: Kwanza kuendelea kuwepo katika ‘game’ hadi leo ni mafanikio. Lakini pia ujue sanaa ndiyo inayoniweka hapa mjini. Hata hivyo natarajia mafanikio makubwa zaidi kwani miongoni mwa malengo yangu ni pamoja na kuwa Director wa Kimataifa na kwa hili nitarudi shule ili niweze kuendesha sanaa kisomi zaidi.
Ten question nitakuwa nawaletea kila siku ya Ijumaa, Endelea kucheki na mateja20 kila kukicha mambo mbalimbali yanapatika humu.


MISS TANZANIA TAYALI KWA SAFARI YA MISS WOLD NCHINI CHINA

Genevive Emmanuel akiwa ameshikilia bendera ya taifa mara baada ya kukabidhiwa rasmi tayari kwa safari yake ya kuelekea nchini China leo.
Vodacom Miss Tanzania, Genevieve Emmanuel Mpangala, jana ikabidhiwa Bendera ya Taifa tayari kwa safari yake ya kuelekea nchini China katika jiji la Sanya ambako shindano la dunia Miss World 2010 inatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu. Genevieve ataondoka leo kwa ndege ya Shirika la Quatar Airways akipitia Uarabuni, Mongolia na kisha kutua Sanya nchini China.


Esther Mkwizu (wa pili kushoto), ambaye ni Mwenyekiti wa Sekta Binafsi na aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa Vodacom Miss Tanzania akikabidhi bendera hiyo huku wazazi wa Genevive wakishuhudia, kulia ni baba yake Bw. Emmanuel Mpangala na kushoto ni mama yake Mary.

DAH!! INASIKITISHA SANA

Hakika kifo hakina huruma wala saa hata notisi.Kilichomtokea mzee huyu leo asubuhi pale pande za Ubungo Bus Terminal kinasikitisha sana. Mzee wa watu, ametoka nyumbani kwake asubuhi na mapema kuelekea kwenye kituo cha mabasi kwenda huko alikokuwa amepanga kuwa mgeni au kureja nyumnani kwake siku ya leo, bila kujua kuwa Mungu amempangia kifo chake leo kabla ya jua kuchomoza. Mzee, huyu ambaye hakutambulika mara moja, amegongwa na basi la abiria liendalo mikoani wakati likitoka lango kuu kwenda na safari zake, tairi lilipanda mwilini mwa mzee huyu na kumuua hapohapo akiwa ameshika mkoba wake wa safari mkononi. Hivi sasa tunavyosoma habari hii ya kusikitisha mwili wake uko mochwari katika hospitali ya Mwananyamala na kwa yeyote anayemfahamu ajitokeze, nahisi familia yake haina taarifa. Mungu alitoa na YEYE ametwaa mja wake, YEYE ndiye Mfalme wa Mbingu na Ardhi na KWAKE sote tutarejea!! Ailaze roho ya Marehemu Peponi - ameen!

umati wa wasafiri na wapita njia wakishuhudia mzee wa watu akiwa hana kauli tena

...basi la kushoto (ambalo halikuweza kujulikana mara moja) ndilo lililohusika na ajali hiyo. Dereva wake alijisalimisha mikononi mwa polisi, ingawa basi liliruhusiwa kuendelea na safari zake.

..askari polisi wakisaidiana na raia kumpakia marehemu garini

...maiti ikipelekwa kuhifadhiwa Mwananyamala hospitali.

WADAU WA MATEJA20KATIKA SWAGGER TOFAUTI

Anajulikana kwa jina la Husna Idd a.k.a Sajenti Kimwana Manywele, hapa yupo ndani ya Boutique yake maeneo ya Sinza Mori jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Johannesburg Hotel Mgini Nyamwelo,wa kwanza kushoto akipekuwa pekua baadhi ya documents kwenye Computer na Receptionist wake Sharifa.
Sajenti katika Swagger tofauti ndani ya 'ki' Boutique chake!!!
Eeh! unaona baanaaaa!
Mgini akiwa bize na Computer yake ndani ya Hotel hiyo.
KUBALI ukatae but ukuweli uko hivi, Bwana mdogo huyu ni mwanamuzi wa muziki wa kizazi kipya na anakwenda kwa jina la Bablee, hapo nyuma aliwahi kutamba na kibao cha Kizizi, akitokea katika lebo ya G2 records. So nachotaka kukuambia dogo huyu huwa ana Swagger za hatari awapo kwenye mambo ya Shouting za kazi zake, Cha ajabu zaidi hivi karibuni nilisikia kibao chake cha ChaguaMoja, kikipigwa kwa fujo katika station mbalimbali za radio imani yangu ni kwamba soon atalejea kenye game tena kwa fujo kali japokuwa simsikii tena.
Bablee katika pozi.
Unaona Swagger zake?
Yaani pozi kama mshikaji yuleeeeeeee !!!!!!!





TAIFA STARS KAMBINI TAYARI KUIVAA MOROCCO


Kocha wa Taifa Stars, Jan Poulsen (kulia) akipata mlo wa mchana.


Kocha msaidizi wa ‘Stars’, Sylvester Marsha (kulia), akiongea kwenye simu wakati wa maakuli. Katikati ni meneja mkuu wa Atriums Hotel, Hudson Msalali, akibadilishana mawazo na makocha hao.

Baadhi ya wachezaji wakichukua chakula muda mfupi baada ya kuwasili hotelini hapo.


Mohamed Banka (wa kwanza kulia) akipata chakula na wachezaji wenzake.


TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars, leo imetua katika hotel ya Atriums iliyoko Sinza-Afrika Sana, jijini Dar es Salaam, kwa maandalizi ya mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika 2012 dhidi Morocco katika mchezo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 9 mwaka katika Uwanja wa Taifa. Kamera yetu ilifika hotelini hapo na kurekodi matukio kadhaa ya timu hiyo.



JULLIET ATUA NA TAJI LA MISS CONGRESS INTERNATIONAL

Jullieth (kushoto) baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Julius Nyerere (JNIA).


Akisali pamoja na familia yake.


Akiongea na wanahabari.




Akimkabidhi bendera aliyokwenda nayo Afisa Habari wa Bodi ya Utalii nchini Miss Immaculate.


Jullieth akiwa kwenye pozi na mama yake mzazi aitwae Rosemary Thadei.

Akiwa na Mkurugenzi wa mashindano hayo hapa nchini, Beatus Kaboja wa kampuni ya Syscorp Managements.

MREMBO Jullieth William, aliyekwenda kupeperusha bendera ya Tanzania nchini Itary, kupitia shindano la Miss Congres Internatinal lililofanyika Ijumaa iliyopita na kufanikwa kutwaa taji hilo kwa kuwa mshindi wa kwanza, leo amewasili hapa nchini na kuikabidhi bendera ya taifa kwa serikali.



Wednesday, September 29, 2010

TANZANIA MODELS KUFANYA ONYESHO LA MAVAZI ARUSHA!!!


KIKUNDI cha Wanamitindo kijulikanacho kwa jina la 'Tanzania Models Group' wanatarajia kufanya onyesho la mavazi katika ukumbi wa Via Via Club jijini Arusha litakalofanyika jumamosi. Akizungumza na Dimba Mratibu wa onyesho hilo lililopewa jina la 'Time and Beauty' Bi. Angel Justace alisema kuwa lengo la kuandaa onyesho hilo ni kuweza kutangaza umoja wao, kuvumbua vipaji vya vijana na kutangaza Utalii wa nchi ya Tanzania. Bi. Angel Justace alisema kuwa kwa sasa wakati umefika kwa vijana kuungana katika kutangaza utalii wa nchi. "Sisi kama vijana hatuna budi kujitoa kwa kuungana na kutangazaa Utalii wa nchi yetu, kwani bila kufanya hivyo nchi yetu haiwezi kutambulika na wageni hawawezi kujua nchi yetu ina vivutio gani vinavyovutia," Onyesho hilo linalotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Via Via Club litawakutanisha wanamitindo kutoka Dar es Salaam na jiji la Arusha huku wakipabwa na mbunifu wa mavazi ya asili Bw. Gabriel Mollel Sairiamu. Aliongeza kuwa mbali na mbunifu huyo wa mavazi ya asili Bw. Gabriel Mollel Sairiamu pia atakuwepo msanii wa kizazi kipya Hussein Machozi. Onyesho hilo limedhaminiwa na Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro Conservation-Arusha, Kilimanjaro Express Bus, Mwandago Evestiment, Coco Pazzo, Triple A Radio na Masai Club ya Dar es Salaam.

P.FUNKY : KIBAO SAWA, ILA SIJAMTOLEA BASTOLA AFANDE SELE,

Producer na mmiliki wa Bongo Records, P.Funky 'majani', ambaye wikiendi iliyopita aliingia katika 'bifu' na Mfalme wa Rhymes Afande Sele, amevunja ukimya na kuongelea tukio hilo. Majani anakiri kumchapa kibao Afande lakini anakanusha kumtolea bastola kama alivyodai Sele na kunukuliwa katika media, Hapa anaelezea kisa kizima na sababu zilizomfanya amuadabishe mfalme huyo wa Rhymes wa Bongo...Bonyeza player msikilize mwenyewe.......

Producer P- Funky 'Majani'

Tuesday, September 28, 2010

CRISS WAMARYA AJIPANGA KI MUZIKI!!!!!!!


CRISS WAMARYA sasa aapa kuja kivingine, katika game ya bongo fleva na kuwapa raha zaidi mashabiki wake. Kwani anasema ladha ya sasa ni kama vanila fleva,Ila kwa sasa kasema tayari kashamaliza kurekodi Audio na Video kwa pamoja na kuwapa raha mashabiki wake.kwa maelezo yake zaidi Criss kasema nyimbo yake inayo kuja kwa jina la kilomita sita, imefanywa katika studio ya ONE MUSIC na video ikifanywa na E MEDIA. Ambayo anatarajia kuitoa video na audio mwezi wa kumi,kwa habari toka kwa criss zinazidi kusema kuwa kazi hiyo itakuwa nzuri zaidi ya nyimbo yake SINYORITA.


Pamoja na hayo yote kamalizia kwakusema anaomba sapoti toka kwa mashabiki wake na wadau wa muziki kwa mawasiliano: +225718777667 or +2257122222 e mail: crisswamarya11@yahoo.com

Monday, September 27, 2010

HAAA!!! SALMA NA MAMBO YA POZIZIIIII


Mrembo, anakwenda kwa jina la Salma.... ni mdau wa Mateja20 so kama vipi nicheki ili nikupe full data zakeeee........ baaaanaaaaaaaaa, maana hana majigambo ni mtu wa watu yaani yu' freeeeeshiiiiiiiiiii!!!!!!!!!!.

KAMA KAWA, KAMA DAWA, POZI NDO KWETU BAANA!!

Siwatajii... kama vipi nanyi jishughulisheni kutafuta ji.... lake baaanaaa!!!
Mambo ya pooozi'ssss..............
Leo sisubutu kutaja hadi nione maoni yenu wazeeeyaaaaaaaaaaa!!
Eeeeh!! wako poa kweli taizo maj.... kuwafaham ndo issue kwa leoooo
Najua hapa mtahisi aliyeachia ta.... la TZ.
Huyu nitawaambia kwakuwa ni mnenguaji wa Twanga, Asha Said 'Shalapova'
Tumeni maoni yenu niwape nambaaaaaaaaaaaaa zao!!
Eti kama mnamfahamuuuuuuuuuuu!!!!!!!!
Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania (kushoto) na mwanaye wakiwa kwenye pozi na mateja20.
Rapa machachali wa Twanga (mwenye miwani) Fagason akifuatiwav na Mateja20 bila kumsahau Said, ambapo tulikutana pande za Leadars Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bonanza la wasanii TZ Michael Sango 'Mac' (Kushoto) Akiwa na mjumbe wa kamati hiyo Dinno (katikati) na mwisho ni Coco mwanamuziki wa FM Aademia.
Wadau wakiwa katika pozi makini wakiongozwa na Cathbert wa Michuzi JR, wa kwanza kushoto.
Fagason aki.... na Anger wake baaaaaaaanaaa!!!!!!!!!
Kama hivi wazeeeeeeeeyeeeeeeey!!
Jopo zima la viongozi wa (TAFF) wakiwa kwenye pozi na Rais wao wa ( mwisho kulia) Saimon Mwakifamba.