Social Icons

Wednesday, June 23, 2010

Vengu, tutemee mate chini

Na Richard Bukos
Ni tukio la kuhuzunisha lililobeba majonzi tele ambapo staa wa Kundi la Orijino Komedi, Joseph Shamba ‘Vengu’, amekumbwa na mkasa mzito ambao umesababisha mashuhuda watoe kauli ya kutemea mate chini.

The 5star Paper, Risasi Mchanganyiko lina ‘full details’ kwamba Vengu, anadaiwa kufanyiwa mchezo mbaya baada ya kugida ‘tingas’ kwa pesa zake za mfukoni lakini mwisho wa sinema alikutwa ‘amejitelekeza’ bila kujitambua, Sinza, Dar.
Staa huyo ambaye ‘hufiti’ zaidi anapoigiza kama demu, alikutwa akiwa hana fahamu, umbali wa mita chache kutoka Klabu ya Sun Cirro, Sinza, alfajiri ya Jumapili iliyopita.

Mapaparazi wetu, ‘walinyetishwa’ kuhusu mkasa huo wa Vengu, Jumapili majira ya saa 5 asubuhi na kufika eneo la tukio ambapo walimkuta staa huyo wa kuwavunja watu mbavu ‘runingani’ akiwa amehifadhiwa nyumbani kwa msamaria mwema mmoja.
Ishu nzima inasimuliwa na mashuhuda kuwa usiku wa kuamkia Jumapili, Vengu ambaye inadaiwa ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa, alionekana akifakamia pombe kwa staili ya ‘kata mti panda mti’ au ukipenda unaweza kuita ‘bandika bandua’.

Mmoja wao ambaye hakutaka jina lake lipambe ukurasa, alidai kwamba mpango mzima wa ‘kutandika maji’ ulifanyika kwenye baa moja ‘bubu’ na aligida hadi usiku mnene ambapo alihamia kiwanja jirani na kuendeleza libeneke hadi alipopoteza ‘netiweki’.
Alifafanua kwamba wakati Vengu anatia ‘maguu’ kwenye baa hiyo alionekana na majeraha mdomoni ambayo haikueleweka yalitokana na nini, ingawa zilikuwepo hisia kwamba alifanyiwa mchezo mbaya.

Mpashaji huyo aliendelea kudai kwamba alipofika kwenye baa hiyo, Vengu aliendeleza makamuzi ya kukata maji hadi alipopoteza ‘netweki’.
“Si unajua tena wikiendi, kila mtu na hamsini zake lakini alfajiri watu ndiyo wakashtukia kumbe jamaa aliangusha gari kwenye kona moja hivi ambayo ilimsababishia kutoonekana haraka,” alisema ‘sosi’ wetu na kuongeza:
“Ile alfajiri katika kumsaidia ndiyo tukamhifadhi kwa huyo msamaria mwema.”

Akizungumza na paparazi wetu, msamaria huyo alisema kuwa baada ya kumpokea Vengu, alitafuta namba ya msanii mmojawapo wa Orijino Komedi ambapo aliipata ya Emanuel Mgaya ‘Masanja’ kisha kumpa taarifa hizo.
“Nilipompigia simu Masanja kumpa taarifa alionesha kukasirishwa na kukemea tabia za mwenzake halafu akakata simu. Baadaye meneja wa kundi lao, Seki (Sekioni David), alikuja kumchukua,” alisema msamaria mwema huyo.

Mara kadhaa Vengu amekuwa akiripotiwa kukutwa na matukio ya aina hiyo ambapo ukiachilia mbali hilo, mwaka jana alizimika na kulala barabarani nyuma ya usukani wa gari.
Kutokana na kupitiwa usingizi akiwa anaendesha, Vengu alisababisha foleni kwenye Barabara ya Shekilango, Bamaga, Dar, hivyo madereva wengine kumpigia honi mfululizo lakini hakuzinduka.

Baadaye, watu walilizunguka gari la Vengu na walipomuona, Seki alipigiwa simu ambaye alifika haraka na kuvunja kioo cha gari, akachomoa ‘loki’ na kuliendesha.
KWETU SISI
Tunamtaka Vengu kubadilika haraka iwezekanavyo kutoka kwenye tabia aliyo nayo ya ulevi wa kupindukia. Pia anahitaji kujitambua kuwa yeye ni msanii ambaye ni kioo cha jamii, hivyo anapaswa kuwa mfano wa kuigwa.

Monday, June 21, 2010

ANNA KIWAMBO anyakua taji la miss tanga 2010


ANNA KIWAMBO anyakua taji la miss tanga 2010
Mnyange wa Miss Tanga 2010 Anna Kiwambo akiwa katika uso wa furaha punde tu baada ya kutangazwa kuwa mshindi katika mchakato huo uliofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort iliyopo Sahare, Miss Tanga 2010 imeandaliwa na 5 Brothers Entertainment.


Mkuu wa mkoa wa Tanga Saidi Kalembo akimpa mkono wa hongera mnyange wa Miss Tanga 2010.

Friday, June 18, 2010

RBP NA TWIGA STARS WALIVYOADHIMISHA SIKU YA 'MTOTO WA AFRIKA’

KAMPUNI ya RBP & Industrial Technology .T. Limited chini ya Rais wake Bi Rahma A. Al-Kharoosi Jumatano wiki hii ilijumuika na watoto zaidi ya mia moja kutoka vituo mbalimbali vya yatima hapa nchini katika kusherehekea Siku ya Mtoto wa Afrika katika ufukwe wa South Beach, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika hafla hiyo Al-Kharoosi alisema ameamua kuwakutanisha watoto katika ufukwe huo ili waweze kufurahi na kucheza pamoja kutokana na mapenzi yake makubwa kwa watoto.

Rahma ambaye pia ni mlezi mkuu wa timu ya wanawake ya taifa (Twiga Stars) aliongeza kwamba siku hiyo ya Mtoto wa Afrika ilikuwa siku nzuri kwake kukaa na timu hiyo kabla ya mchakato mpya wa kwenda kuwania fainali za Kombe la Afrika zitakazofanyika Afrika Kusini mwezi wa kumi mwaka huu.


Rahma A.Al-Kharoosi (kulia) akibadilishana mawazo na baadhi ya wachezaji wa Twiga Stars katika ufukwe wa South Beach katika Siku ya Mtoto wa Afrika


Mpipga picha wetu Musa Mateja (kushoto) akiwa katika pozi na mwanamitindo maarufu nchini,
Fidelina Iranga


Mwandaaji wa hafla hiyo, Al-Kharoosi (wa pili kushoto) akifurahia jambo na watoto yatima; wengine ni baadhi ya walezi wa watoto hao


Baadhi ya viongozi wa kampuni hiyo na walimu wa watoto waliohudhuria sherehe hizo wakiwa kwenye picha ya pamoja.



Meneja mkuu wa RBP & Industrial Technology.T. Limited, Ibrahim Khatrush (kushoto), akiwa na kaka yake, Mohamed Khatrush, ambaye ni meneja wa kampuni ya London Mine Camp iliyo chini ya kampuni hiyo.


Mmoja wa watoto yatima akilishwa chakula na Bi Al-Kharoosi katika sherehe hizo.


Nahodha wa Twiga Stars, Sophia Edward Mwasikili, akiongea na waandishi wa habari siku hiyo.


Ibrahim Khatrus mwenye miwani akijipatia chakula.


Rais wa Kampuni hiyo naye hakuwa nyuma kujichukulia msosi mahali hapo.


Rais wa RBP akipiga ‘cheers’ na mmoja wa watoto yatima.



Fideline Iranga akijaribu kupekuwa habari kwenye kompyuta yake na rafiki yake, aliyejulikana kwa jina moja la Martin.


Bi Al-Kharoosi akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya timu nzima iliyokuwepo katika hafla hiyo.



Sophia Edward (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mlezi wa timu hiyo, Bi Rahma Al-Kharoosi, na wa mwisho kulia ni mmoja wa wachezaji wa timu hiyo.







Wednesday, June 16, 2010

TINNO AKIWA NA SHAMSA KATIKA POZI ZITO

NANCY SUMARI AKIWA NA IRENE KIWIA

MATEJA20 AKIWA NA AUNT EZEKIEL

MLIMANI CITY SASA KAMA SAUZI!

Mashabiki lukuki wa soka nchini usiku wa kuamkia leo waliigeuza mlimani City kama Afrika Kusini ‘Sauzi’ baada ya kufulika kwenye viwanja hivyo kutazama mpira kati ya timu ya Taifa ya Brazir na Korea Kaskazini



Sunday, June 13, 2010

TANZANIA MITINDO HOUSE YAZINDUA KITUO CHA KUCHEZEA WATOTO YATIMA

KAMPUNI ya Mitindo House leo iimefanikisha sherehe ya Uzinduzi wa Kituo cha kuchezea watoto yatima iliyofanyika Mwera Manispaa ya Temeke ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Oil &Industurial Technology T.LTD. Rahma A. Al-Kharoosi.

Akiongea katika ufunguzi huo Mwenyekiti wa Mitindo House Khadija Mwanamboka alisema kwamba wamelazimika kufungua kituo hicho kutokana na uhaba mkubwa wa sehemu za kuchezea watoto yatima hapa nchini na vile vile amekuwa akitafuta namna ya kuwakutanisha pamoja watoto hao ili waweze kujumuika na kucheza pamoja.

Naye Rais wa Oil &Industrial Technology T. Limited Rahma Al-Kharoosi alisema kuwa kampuni yake ilmelazimika kudhamini ishu hiyo kutokana na kuguswa kwake siku nyingi na kwamba hadi sasa iko kwenye mchakato wa kuwakutanisha watoto sehemu moja hasa siku ya watoto Duniani ili waweze kula na kufurahi pamoja.

Mgeni Rasmi Rahma Al-Kharoosi (Kushoto) akipokelewa na Mwenyeji wake Khadija Mwanamboka muda mfupi baada ya kuwasili eneo hilo.

Rahma Al-Kharoosi (katikati) akifungua ubao unaoonyesha jina la Kituo hicho kulia kwake anayeshuhudia zoezi hilo ni Meneja wa London Mine Camp Mohamed Khatrush akiwa na baadhi ya watoto na wageni waliohudhulia shughuli hizo.

Khadija Mwanamboka (kushoto) akimpa mkono wa pongezi mgeni Rasmi baada ya kumaliza zoezi la ufunguzi.

Mgeni Rasmi akiwa amekumbatiana na mmoja wa watoto yatima waliokuwepo katika shughuli hizo.

Baadhi ya watoto wakijaribu kuimba na wimbo na mgeni rasimi muda mfupi baada ya kuzindua mpango huo.

Rahma Al-Kharoosi aliyebeba mtoto akibembea na watoto katika moja ya Bembea zilizopo mahari hapo.

Mwenyekiti wa kituo hicho (kulia) akionyesha tano kwa furaha na mgeni rasmi muda mfupi baada ya kuhitimisha zoezi la ufunguzi wa ishu hiyo.

Fiderene Iranga (kushoto)akibadilisha mawili matatu na mmoja wa wageni waarikwa waliyohudhuria uzinduzi huo.

Mgeni rasmi akionyesha aina ya chakula anachokipenda mara baada ya kukaribishwa kupata msosi.

Thursday, June 10, 2010

ZAIN YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA JIVUNIE SMS


Kampuni ya Simu za Mkononi ya Zain leo imekabidhi jumla ya shilingi milioni moja (1,000,000) kwa washindi wawili wa Promosheni ya Jivunie SMS.Washindi waliokabidhiwa zawadi zao za pesa taslimu leo ni wale waishio jijini Dar es Salaam, wakati washindi waishio nje ya jiji la Dar es Salaam watakabidhiwa zawadi zao hivi karibuni.

Akiwataja washindi waliojizolea kitita cha laki tano kila mmoja, Meneja Masoko wa Zain Tanzania Constantine Magavilla, alisema ni Mashimba Mashimba mkazi wa Tabata Kisiwani jijini Dar es salaam na Philipo Masonda, Osole David Gilina na Godwin Joseph.

Meneja Masoko wa Zain Tanzania, Constantine Magavilla (kulia) akimkabidhi kitita cha sh.500,000/= Philipo Masonda ndani ya makao makuu ya ofisi za Zain Morocco jijini Dar es Salaam.


Mshindi wa Jivunie SMS Mashimba Mashimba akipokea kitita kiasi chake kutoka kwa Constantine Magavilla makao makuu ya Zain Morocco jijini Dar es Salaam



Washindi wote wawili wakiwa wameshikilia pesa zao kwa tabasam muda mfupi baada ya kukabidhiwa.



ADAMU MCHOMVU: DEMU WANGU ANA WIVU ILE MBAYA!


Leo katika pande hizi tunakudondoshea presenta mwenye heshima kubwa kwa vijana ‘anayehosti’ programu ya XXL kunako Redio ya Watu, Clouds FM, Adamu Mchomvu ‘Brother from another Mother’.
Huyu jamaa alizaliwa miaka 26 iliyopita huko Kahama mkoani Shinyanga, lakini akakulia kwa ‘machalii’ Arusha maeneo ya Silentini Sakina ambapo aligonga Primary katika Shule ya Meru kabla ya kujiunga na Sekondari ya Kaloleni, zote za mkoani Arusha. Kutoka hapo Adamu alikwenda kugonga ‘five na six’ nchini Uganda katika Shule ya Ntinda View iliyopo katika Jiji la Kampala. Ili kujua ‘in and out’ ya Brother from another Mother, tuungane katika sindano kumi za maswali ya moto.

TQ: Unaweza kukumbuka ni lini na ilikuwaje ukajiunga na fani ya utangazaji?

ADAMU: Utangazaji nilianzia Uganda na stori nzima ilikuwa hivi; Ilitokea noma pale skuli nikatimuliwa baada ya kuingilia ugomvi wa mademu wawili mmoja kutoka Bongo. Katika lile soo nilikuwa nawaamulia wale mademu ndipo mtangazaji mmoja aliyeitwa Isack akasikia sauti yangu na kunifuata kisha akanitaka nifanye Tangazo la Vicks Kingo ambapo nilipoteza mbaya. Baada ya hapo nilipata chansi ya kuruka hewani na kipindi changu cha burudani katika chaneli ya Redio ya Green FM ya nchini Uganda. Baadaye nilirudi nyumbani na kuwaeleza wazazi stori ilivyokuwa na wakaniruhusu kufanya kile kilichokuwa moyoni.

TQ: Baada ya hapo ilikuwaje hadi hapa ulipofikia?
ADAMU: Nilipotimba Dar nilijiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari cha DSJ ambapo nilisomea Diploma ya fani hiyo, lakini kabla sijamaliza Clouds FM waliniona na wakanichukua na ndiyo unaniona kama hivi nakimbiza ile mbaya.

TQ: Kazi yoyote ina vikwazo vyake. Je, wewe ni mambo gani unakutana nayo yanakunyima kupiga mzigo ili kufikia malengo yako?
ADAMU: Unajua watu wananichukulia tofauti, mara najisikia, naringa, ukipanda bajaj umefulia na mengine yanayofanana na hayo yanayosababishwa na umaarufu.

TQ: Usumbufu wa Mademu vipi?
ADAMU: Kusema kweli usumbufu ni mkubwa. Kwa siku naweza kupokea meseji zaidi ya kumi za mademu wanaotaka niwe nao ‘but’ mimi huwa nawapigia kimya ‘coz’ nina demu mwenye wivu ile mbaya.

TQ: Wewe unahusika na kuwapromoti maandagraundi, Je, usumbufu ukoje?
ADAMU: Hawa jamaa wanaishia tu kueneza lawama kwamba sisi ni wabaya na tunawabania, lakini ukweli ni kwamba pale ofisini kuna utaratibu wa kupokea kazi mpya na kuzikiliza kisha kuzipeleka hewani, sasa jamaa ukiwaelewesha hawaelewi kabisa, wanaona mimi ndiyo mbaya wao.

TQ: Kuna tuhuma kwamba mnaweka kapuni baadhi ya kazi za wasanii na wengine mnawapa promo, je, hii ikoje?

ADAMU: Kama nilivyoeleza awali hakuna kitu kisicho na utaratibu. Wengine ukiwaambia wafuate utaratibu wa kuleta kazi zao zisikilizwe kwanza ndipo ziende hewani, hawataki na badala yake wanaishia kulalama na kueneza mbovu mbovu kitaa.

TQ: (swali la kifuta jasho) Umeoa? Na kama bado, utaoa lini?
ADAMU: Sijaoa ila nina wangu. Muda wa kuoa ukifika nitasema but siwezi kusema lini.

TQ: Mafanikio vipi?
ADAMU: Nina gari, ploti mbili Arusha na Dar. Nina uwezo wa kubadili jinsi (suruali) na msosi ‘so’ namshukuru Mungu.

TQ: Baadhi ya mastaa Bongo ni zoa zoa wa mademu, hii kwako imekaaje?
ADAMU: Hayo mambo mimi sina kabisa mzazi.

TQ: Nini matarajio yako ya baadaye?
ADAMU: Nina mpango wa kuja kumiliki kampuni moja kubwa sana ya burudani.