MAD ICE KUWAPIGA JEKI WASANII WA KIBONGO
Na Erick Evarist
MSANII wa longtime ndani ya gemu la muziki wa kizazi kipya nchini, Mad Ice juzikati aliahidi kuwasaidia wasanii kibao wa kibongo kulisongesha mbele gurudumu la muziki wa Bongo Fleva.
Akipiga stori mbili tatu na Paparazi wetu hivikaribuni maeneo ya Millenium Towers Kijitonyama jijini Dar es Salaam, alisema kwamba mara atakapo rejea maskani kwake anakuishi kwa sasa nchini Finland, atahakikisha anatangaza kazi mbalimbali za kimataifa kupitia mtandao wake na wabongo wengi watapata kutangaza kazi zao kupitia mtandao wa kampuni hiyo.
“Nimegundua kuna vipaji vingi
“Kuna vipaji vingi chipukizi ambavyo tukiungana na kujitangaza pamoja katika soko la kimataifa nadhani tutafika tunapohitaji maana
Utaratibu mzima wa namna ambavyo wasanii watatakiwa kutuma kazi zao sikilizia hapa hapa tutakulisha.
0 comments:
Post a Comment