Social Icons

Friday, January 28, 2011

MIYEYUSHO NA FUNDI KUKAMUANA KESHO


Bondia Juma Fundi (kushoto) akipimwa afya kabla mpambano.
MABONDIA Francis Miyeyusho na Juma Fundi, kesho wanatarajia kupambana katika mchezo wa raundi 10 utakaofanyika katika Ukumbi wa Amana Vijana Social Jijini Dar es Salaam. Leo mchana paparazi wetu aliwanasa mabondia hao ukumbini hapo wakiwa kwenye hatua za mwisho za mpambano huo ikiwemo kupima afya zao.



Francis Miyeyusho (kushoto) na Fundi wakitunishiana misuli.

Promota wa pambano hilo, Kaike Siraj (katikati) akiwainua mikono juu mabondia hao kuwatakia mchezo mwema.

Aliyewahi kuwa mshindi wa Shindano la Bongo Star Search (BSS),Jumanne Idd naye alinaswa eneo la tukio na kudai atawatumbuiza mashabiki kabla ya mpambano huo.

0 comments: