Huduma hiyo imezinduliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Dk Patric J. Makungu katika hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam.
Mtandao huo, kwa mujibu wa Tigo, unatumika katika simu za aina ya Blackberry na laini za Tigo tu.
Dk Makungu amesema kuwa hayo ni matokeo mazuri ya utekelezaji wa sera za serikali ambazo kwa ujumla wake zinalenga kuweka mazingira mazuri ya ushindani na ubunifu katika sekta binafsi ambayo wananchi wanashuhudia kupitia uboreshwaji wa huduma na kupungua kwa gharama za huduma zinazotolewa.
Aidha amesema kuwa viwangio vya chini vilivyowekwa na kampuni ya Tigo katika vifurushi vya huduma hii ya Blackberry ni ushuhuda wa jinsi kampuni ya Tigo ilivyojipanga na kutumia fursa hiyo vizuri.
Kwa upande wake Ofisa Mwendeshaji Biashara Mkuu, Diego Gutierrez, alisema mtandao huo una kasi kubwa kwa mawasiliano na kwamba wateja wake watafurahia huduma hiyo.
Guitierrez alisisitiza kwamba huduma hiyo itakuwa na gharama ndogo ambayo itawawezesha wateja kuwasiliana kwa barua-pepe, kuwasiliana kuhusu hafla mbalimbali na kuwasiliana katika maongezi binafasi, na kadhalika.
Mshereheshaji wa shughuli hiyo, Denis Busulwa ‘Ssebo’, akiwajibika.







Baadhi ya vyakula vilivyokuwa vimeandaliwa katika hafla hiyo.
0 comments:
Post a Comment