Social Icons

Wednesday, September 15, 2010

HOTPOT FAMILY WARUDI KWA KISHINDO!!!

Kundi zima katika pozi.
KUNDI zima la muziki wa Kizazi kipya nchini la Hot Pot Family, kutoka pande za Kalakata Air port jijini Dar es Salaam, Hatimaye limetangaza nia yake ya kurejea kwenye game kwa kishindo likiwa limekumbatia Single mpya inayokwenda kwa jina la Unamipango, ambayo imekaangwa na kuivishwa katika Studio za MAKAVELI chini ya Producer Muba Touch.
Akiongea katika mahojiano mafupi na Mateja20 mmoja wa wahasisi wa kundi hilo Suma G, alisema kwamba awamu hii wamezamilia kufanya makubwa katika game la muziki wa Bongo, na kwamba tayali wameshaongeza safu ya washambuliaji na kundi kufikia idadi ya watu 8 tofauti na ilivyokuwa mwanzo.
Uboreshaji huo Suma G, alidokeza kwamba kutokana na mpango mzima wa kutobagua jinsia wamempa shavu mrembo mmoja ambaye watakuwa naye katika halakati za kusongesha kundi hilo hivyo suma G alitumia fursa hiyo kuwaomba wadau wote wa muziki huo wakae makao wa kula tayari kwa mapambano kutoka kwao.

0 comments: