Social Icons

Thursday, August 26, 2010

BABY MADAHA AMNYAKA GERRY

Staa wa kike mwenye heshiuma tele katika Bongo Flava, Baby Joseph Madaha, ameendelea kuzua minong’ono kibao kwa jamii kutokana na ukaribu aliyonao na msanii chipukizi mwenzake, Elius George ‘Gerry’, Mateja20 haipitwi.
Kwa mujibu wa sosi makini wa Amani, habari kubwa iliyozagaa kitaa ni kwamba Baby kwa sasa amemnasa chipukizi huyo aliyeshirikishwa kwenye ngoma ya Mama Ntilie inayosumbua katika runinga na redio mbalimbali.
Inaelezwa kuwa Baby amekuwa akionekana ‘vere klozi’ na dogo huyo, jambo linalosababisha kuenea kwa ‘rumansi’ hizo kama moto wa kifuu.
Kama kawa kama dawa, baada ya kuinyaka ishu hiyo, Mateja20 ilimuinulia mkonga wa simu Baby na kumsomea ‘eituzedi’ ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Jamani jamani, yule kweli ni rafiki yangu lakini siwezi kuvunja naye amri ya sita kwenye vitabu takatifu.”

0 comments: