Social Icons

Wednesday, November 2, 2011

Kamanda Henry Kilewo, Katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda ya Dar es salaam, aliyesoma tamko kali la CHADEMA jana.

MKOA WA KINONDONI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM

Tamko la katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum ya Dar es salaam

Ndugu zangu wanahabari,

Nimewaita hapa leo kwa lengo la kuwapa watanzania msimamamo wangu na wa chama ngazi ya mkoa kuhusu tukio la kukamatwa na kupelekwa magereza kwa Mhe. Godbless Lema Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini.
Imekuwa ikizoeleka kwa muda mrefu sasa kwamba waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na wale wanaaotokana na vyama vya upinzani wamekuwa wakinyanyaswa sana kwa lengo la kuwafanya wajute kuingia katika siasa za upinzani Tanzania.

Hii kwa…

MKOA WA KINONDONI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM

Tamko la katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum ya Dar es salaam

Ndugu zangu wanahabari,

Nimewaita hapa leo kwa lengo la kuwapa watanzania msimamamo wangu na wa chama ngazi ya mkoa kuhusu tukio la kukamatwa na kupelekwa magereza kwa Mhe. Godbless Lema Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini.
Imekuwa ikizoeleka kwa muda mrefu sasa kwamba waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na wale wanaaotokana na vyama vya upinzani wamekuwa wakinyanyaswa sana kwa lengo la kuwafanya wajute kuingia katika siasa za upinzani Tanzania.

Hii kwa CHADEMA haitokei tu kwa waheshimiwa wabunge bali hata kwa viongozi wa ngazi zote. Inaonekana kuwa sasa serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeamua kutekeleza kwa vitendo mkakati wa kuwatesa kwa siri na kwa wazi wale wote wanaoipinga siasa kandamizi na zisizowalazimisha watawala kuwajibika kwa wananchi.

Mkakati huu umetungwa na CCM, unasimamiwa na usalama wa taifa na unatekelezwa na jeshi la polisi. Kwa hakika hatuhoji tena kwamba jeshi la polisi ni kitengo cha kusimamia maamuzi na maelekezo ya CCM badala ya kulinda raia na mali zao.

Mheshimiwa Godbless kama mbunge wa wananchi wa jimbo la Arusha Mjini amekuwa akifuatwafuatwa na jeshi la polisi kila mara na kufanyiwa vitendo vingi vya udhalilishaji na unyanyasaji hasa kwa kupitia OCD wa Arusha Mjini Zuberi.

Mathalani wiki iliyopita siku ya ijumaa tarehe 28/10/2011 Mhe. Godbless lema akitoka mahakamani alisindikizwa na wananchi wake kutoka mahakamani hadi ofisini kwake. Wafuasi wake walipomfikisha ofisini waliondoka na kurejea makwao. Huko ofisini aliwakuta wananchi wakimsubiri ili awahudumie kama mbunge wajimbo lao. Wakati akiongea na wananchi ghafla polisi walifika na kuwakamata wananchi wote waliokuja kuomba usikivu wa mbunge na kuwapeleka kituo kikuu cha polisi.

Mbunge Lema alipokwenda kituo cha polisi kwa lengo la kuwawekea dhamana naye aliwekwa chini ya ulinzi kwamba eti amefanya maandamano bila kibali.

Tunahoji: Ni maandamano yapi hayo ambayo Lema aliyafanya na wananchi wake akiwa angali ofisini kwake? Je maandamano wanayoyazungumzia ni kuondoka na wananchi mahakamani hadi ofisini kwake? Je kama kuondoka kwake na wafuasi wake mahakamani ni kosa kisheria; Je kwa Mhe Ole Sendeka alipokuwa akitoka mahakamani, alikuwa akiondoka na kundi kubwa la wafuasi wake na kusindikizwa na OCD huyu huyu? Vile vile Mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Arusha amekuwa akienda kituo kikuu cha polisi akisidikizwa na kundi kubwa la wafuasi wake wa CCM. Polisi hawakuwahi kuwakamata wala kuwaonya. Sasa haya yote yalikuwa maandamano ama matembezi ya hisani? Maana Arusha kuna msiba mkubwa wa CCM kukataliwa na wananchi.

Kwa hakika tukio la kukamatwa kwa Mhe Lema, kupelekwa mahakamani na hatima ye kupelekwa gerezani ni ushahidi wa kutosha kwamba jeshi la polisi sasa linakamilisha sehemu kubwa wa wajibu wake wa kuibaka demokrasia.


Hata hivyo tunalitaka jeshi la polisi na serikali ya CCM wajue kwamba kitendo cha kumpeleka Lema magereza ni ushindi tosha katika harakati za ukombozi wa taifa hili. Maana hakuna silaha yoyote duniani ama jeshi la polisi popote pale duniani ambavyo viliweza kushinda vita dhidi ya ukweli, haki na uwazi.

Ndugu zangu watanzania

Tunawaunga mkono wana Arusha kwa kumpata mbunge ambaye anayatetea maslahi yao kwa mzigo hata pale inapobidi kwenda gerezani kwa ajili ya watu wake na hata ikibidi kifo anaweza kusimamia hilo. Alisema Martin Luther King Jr. 1963 “A man who wont die for something is not fit to live” na akaendelea kusisitiza “Nobody can give you freedom, nobody can give you justice or right or anything.

You take it!” (STAND UP; STAND UP 4, UR RIGHT) Hayo yalikuwa maono ya bob marley ambayo aliyaona mwaka wa 1973,baada ya kuwa amekaa katika mto mmoja huko jamaica akaona samaki wanapita katika maji lakini samaki wakubwa wakawa wanawaonea samaki wadogo,hivyo akaona hata hapa duniani hata wa2 walio juu wanawaonea watu wa hali ya chini.

Kwa watu wanaopinga ama kukejeli maamuzi ya Godbless lema kukataa dhamana, Wathubutu kufanya ziara huko Mahospitalini wavae sura za uhasilia wa kibinadamu wakaone watu waliokuwa kama wao jinsi wanavyotaabika kwa kukosa matibabu ile hali ni walipa kodi wa taifa hili. Kwanini Godbless asiende jela wakati anasimamia mambo ya msingi na hayatekelezwi, tukiandamana tunaonekana tunavunja sheria ni afadhali kwenda sehemu wanayodhani tunaogopa kuliko kukaa kimya kumbe hatuogopi. Mungu yupo upande wetu na tunaelekea kushinda unyanyaswaji huu.

Kama ambavyo alivyowahi kusema Martin Luther king jr, ndivyo tunavyo wahakikishia wana wa Arusha, we will work together; we will stand up together, we will go to jail together, until justice runs down like water. maana mateso tunayoyapata ni makubwa kuliko huko jehanam tusipopajua.

Kwa kuonyesha tuko pamoja katika harakati hizi za kudai demokrasia ya kweli tunampogeza Godbless lema mbunge wa Arusha mjini kwa kupeleka ujumbe kwa watawala wanaodhani wanaweza kutumia magereza kama sehemu ya vitisho kurudisha harakati zozote zile nyuma.


Ujumbe huu uwafikie watawala yakuwa jela sisehemu ya kumtishia mtu yeyote Yule mwenye akili timamu, mpenda haki bali ni sehemu ya kawaida ambapo binadamu yeyote Yule anaweza kwenda.

ASANTENI ASANTENI NA MUNGU AWABARIKI WATANZANIA WENZANGU!

Henry J Kilewo
KATIBU (M) Kanda Maalum
01/11/2011


0 comments: