Social Icons

Monday, October 31, 2011

KOCHA WA TIMU YA VIJANA YA MANCHESTER UNITED AANZA KUFUA VIWANGO VYA VIJANA WA AIRTEL RISING STARS BONGOKocha wa soka ya vijana kutoka Manchester United, Paul Bright akionyesha kwa vitendo namna ya kusakata kabumbu wakati wa mafunzo ya kliniki ya soka ya kimataifa ya vijana ya 'Airtel Rising Stars' yaliyoanza jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es salaam. Katikati ni Graham Naftali na Samir Omary (kulia).


Mkufunzi mkuu wa kliniki ya soka ya kimataifa ya vijana ya 'Airtel rising Stars', Billy Miller kutoka klabu ya manchester United ya Uingereza, akijadili jambo na kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Vijana ya Tanzania, Kim Poulsen, wakati wa mafunzo hayo yaliyoanza jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.




Mshiriki wa kliniki ya soka ya kimataifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, Naomi Njeri akimtoka mshiriki mwenzake Emily Auma wakati wa mafunzo ya kliniki hiyo yaliyoanza jana kwenye Uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.


MKUFUNZI mkuu wa kliniki ya soka ya kimataifa ya vijana ya 'Airtel rising Stars', Billy Miller kutoka klabu ya manchester United ya Uingereza juzikati alianza rasmi zoezi la kutoa mbinu hizo kuwawezesha wachezaji kujiamini na kujifunza kutokana na makosa
. Katika siku ya kwanza wachezaji walifundishwa mbinu za kiufundi na stamina
. Wachezaji hao nyota walihudhulia na kushuudia mechi ya ligi ya ndani
Dar es Salaam, Tanzania, 31 Oktoba,2011...Kliniki ya Airtel Rising Stars imeanza rasmi Jumapili 30 Oktoba 2011, huku wakufunzi wakiwataka washiriki kuiga mbinu zinazofundishwa na kutumiwa shule za mafunzo ya soka za Manchester United.
Mafunzo hayo yanayojumuisha wachezaji 16 yatazingatia maendeleo ya kila mchezaji kwa kuzingatia vipengele vitano muhimu ambvyo vitawafanya kuwa wachezaji waliokamilika. Makocha hao kutoka Manchester United walielezea vipengele hivyo kuwa ni uwezo wa kiufundi, uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka uwanjani, kujenga mwili na saikolojia.
Akizungumzia kuhusu program ya kliniki, Kocha Mkuu wa kliniki hii kutoka shule za mafunzo ya soka za Manchester United ambaye ndiye msemaji wa kliniki hiyo - Bw. Billy Miller - alisema mpango wa Manchester United unawafanya wachezaji kuwa huru na kufanya kocha na mchezaji kuwa karibu zaidi, kufanya kazi kwa pamoja ili kutimiza malengo yao.
'Mtindo huu wa ufundishaji humfanya mchezaji ajione ni mtu muhimu na wa kipekee na kumpa hamasa ya kuwa na shahuku ya kujiendeleza zaidi, na kufanya mchezaji kuwa na ali ya kujifunza kutokana na makosa pamoja na tabia na mwenendo akiwa ndani au nje ya uwanja.' Alisema Bw. Miller.
Siku ya kwanza ya kliniki hiyo kwa wachezaji hao ililenga zaidi kwenye ufundi na jinsi ya kumkabili mpinzani wakati wa mchezo na badaye kuhudhuria mafunzo ya darasani yenye kichwa cha habari - jinsi ya kuwa mchezaji mkubwa-. Hii ilitoa fursa kwa makocha na wachezaji kuzoeana na kwa pamoja wakapitia majina ya wachezaji wakubwa duniani na sehemu zao za uchezaji ndani ya uwanja.
Kwenye upande wa ufundi wachezaji walifundishwa mbinu za kumiliki na kupasiana mpira. Wachezaji walingawanyika makundi madogo, ambayo yaliwawezesha wachezaji kupeana pasi nyingi, jinsi ya kusubiri pasi baada ya kutoa na kujijengea uwezo wa kujiamini kupokea pasi hata ukiwa kwenye mazingira magumu kutoka kwa mpinzani.
Wachezaji hao 16 walichanguliwa kutoka kwenye michuano ya Airtel Rising Stars ambayo ilichezwa kutoka kwenye ngazi ya mkoa hadi ya taifa na kuhitimishwa kwa kliniki hii ambayo imeandaliwa Gabon na Tanzania. Nchi ambazo zinashiriki kwenye kliniki hii ya Dar es Salaam ni Tanzania, Kenya, Malawi na Sierra Leone.





0 comments: