Social Icons

Monday, October 31, 2011

ILIVYOKUWA SIKU YA MECHI YA SIMBA NA YANGA KWA MASHABIKI UWANJANI HAPO!!!

Mashabiki wa yanga, wakiingia kwa mbwembwe uwanja wa Taifa huku wakiwa na bendera yenye picha ya mtani wao wa Jadi ambapo furaha hii ilidumu hadi mwisho wa mchezo huo baada ya mnyama Simba kuchinjiwa mbali.
Mashabiki wa Timu ya Simba, wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na maneno yanayoashiria endapo wangeifunga yanga basi kocha wa Yanga Papic angeenea katika nyumba hiyo tayari kwa mazishi jambo ambalo liliwageukia wao na kujikuta kocha wao Timbe, likimzika.

0 comments: