Social Icons

Wednesday, October 26, 2011

ILIKUWA HIVI ZIARA YA WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI KAGERA

Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume (kulia), akiwaongoza wakuu wa vyombo vya habari kutembelea kiwanda cha sukari cha Kagera mwishoni mwa wiki iliyopita. Ziara hiyo ilifadhiliwa na NSSF ili kuona miradi mikubwa ya kiuchumi inayokopeshwa na mfuko huo wa jamii.
Meneja wa kiwanda cha sukari cha Kagera, mhandisi Nestory Rwechungura akiwaeleza wakuu wa vyombo vya habari jinsi kiwanda chake kinavyofanya kazi.
Wakuu wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakipata maelezo ya kitaalamu juu ya mafanikio makubwa ya kiwanda cha sukari cha Kagera katika umwagiliaji toka kwa meneja umwagiliaji wa kampuni hiyo, Laizer Morumo wakati wa ziara yao kiwandani hapo.

0 comments: