Social Icons

Saturday, September 24, 2011

USAHILI WA SHINDANO LA JENGA NCHI YAKO WARINDIMA THE ATRIUMS HOTEL LEO Majaji wa shindano la Jenga nchi yako, wakifuatilia kwa makini namna wasanii wanavyoonyesha uwezo wao, anayeongea wa pili kutoka kulia ni mmiliki wa studio ya Tattoo Record Bw. Faraja Kiobya, akiwa na majaji wenzake Steven Joseph 'Jobiso' (wa kwanza kulia), na Deogratius Manegella 'Dessamo' (kushoto), anaemfuatia ni Annaclara Aidan 'ACM', mchujo huo unaendelea kufanyika ndani ya Ukumbi wa The Atriums Hotel iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa washiriki wa shindano hilo Sianah Jordan (kushoto), akionyesha uwezo wake mbele ya majaji.
Sianah, akiimba kwa hisia kali.
Mshiriki wa shindano hilo Ramadhan Rajab Jumbe (kushoto), akimimina 'song' zake kwa majaji hao.
Ramadhan akitetea nafasi yake.
Mshiriki wa shindano la Jenga Nchi yako Steven James (kulia), akiwajibika mbele ya majaji katika hotel ya The Atriums Sinza afrikasana jijini Dar, leo hii.
Washiriki wa shindano hilo wakiwa mbele ya majaji wa mchakato huo jana ambapo usahili huo ulianza.
Washiriki wakisubilia interview .
Mmoja wa washiriki hao akichalaza gitaa kugombea nafasi hiyo.
Majaji kazini.
Washirika wakisubilia kuitwa majina tayali kwa makamuzi
Mrembo akichana mistari yake kwa majaji.
Mambo yalikuwa hivi The Atriums Hotel.
Mwanaume kazini.
Hisia ndiyo Swagger zenyewe.
Eeee ... razima kieleweke.


SHINDANO la kusaka vipaji la Jenga Nchi Yako, ‘JNY’ limeanza kupiga hatua baada ya mchakato wa awali wa usaili kuanza kwa kuwachuja wasanii wenye vipaji katika hatua ya kuwapata wasanii wenye sifa.

Usaili huo ulianza tangu jana ndani ya Hoteli ya The Atriums Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam, ambapo washiriki hao walionesha vipaji halisi na kusababisha usili huo kuwa wakiushindani zaidi kwa kila mmoja kuwania nafasi ya ushindi.

Akizungumza na MATEJA20 Mratibu wa kinyanga’anyiro hicho, Richard Mathew Manyota ambaye pia ni Balozi wa Amani na Ulinzi Shirikishi Tanzania alisema, kwa sasa shindano hilo linaelekea pazuri kwa kuwachuja wasanii hao na mwisho wa siku kuwapata wale wenye sifa. Manyota aliongeza kuwa anashukuru kwa ushirikiano waliouonesha washiriki hao tangu mchakato huo ulipo anza hapo jana.

“kwa sasa mambo yanazidi kuwa mazuri kani hatua hii inaashilia matokeo mazuri na lengo letu la kuinua vijana wenye vipaji vya kuimba litatimia” alisema Manyota.





0 comments: