Social Icons

Thursday, September 29, 2011

TANO BORA YA BSS 2nd CHANCE 2011, YAGONGA SHOO NA BENDI YA TWANGA PEPETA BILICANAS Washiriki wa shindano la Bongo Star Search Second Chance 2011, walioingia kwenye nafasi ya tano bora, wakiwa kwenye pozi na wanenguaji wa Bendi ya African Stars International 'Twanga Pepeta', muda mfupi baada ya kuingia katika Ukumbi wa Bilicanas Club, tayari kwa makamuzi ya pamoja na bendi hiyo.

WASHIRIKI wa shindano la Bongo Star Search Second Chance 2011, usiku wa kuamkia leo, walifanya shoo ya pamoja na Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’ ndani ya Ukumbi wa Bilicanas, ambapo walienda kwaajili ya kujifua zaidi kufuatia ugumu wa shindano hilo lililofikia kwenye hatua ya tano Bora. ambayo inamalizika wiki hii na mshiriki mmoja kati ya watano ataaga mashindano na kubaki washiriki wa nne, washiri hao walizama ukumbini hapo muda mfupi baada ya kutoka kurekodi kipindi kinachorusha matukio ya shindano hilo kupitia kituo cha Runinga cha ITV, katika Ufukwe wa Mbaramwezi Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Washiriki walio kwenye Tano Bora ni Bella Kombo, Haji Ramadhan, Chiby Dayo, Waziri Salum na Rogers Lucas.



Wanenguaji wa Bendi hiyo wakitumbuiza jukwaani hapo.
Mnenguaji wa bendi ya Twanga Pepeta Lilian Tungaraza ‘Lilian Internet’ (katikati), akiwa kwenye pozi na baadhi ya washiriki wa BSS, Haji Ramadhan (kulia), na Rogers Lucas.
Waziri Salim (kulia), na Rogers Luicas (katikati), wakiwa kwenye pozi na wanenguaji wa bendi hiyo, Maria Soloma na Phasha
Chibby Dayo, Waziri Salim, wakijenga mapozi namna hiyo kwa warembo hao.

Washiri wa BSS, wakiimba jukwaani hapo.


Mshiriki wa BSS, Bella Kombo akiomba kura kwa mashabiki wa bendi hiyo kwa njia ya kuimba.


Kiongozi wa bendi hiyo Luiza Mbutu (katikati), akiwa kwenye pozi na washiriki hao.


Luiza Mbutu (katikati), akiwa katika pozi na washiriki hao.


Mratibu wa shindano la Bongo Star Search Second Chance 2011, (BSS), ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Benchmark Production, Rita Paulsen 'Madam Rita' (kushoto), akiwa katika pozi na mmoja wa washiriki wa shindano hilo Chiby Dayo, muda mfupi baada ya kumaliza kurekodi kipindi hicho katika Ufukwe wa Mbalamwezi Mikocheni jijini Dar es Salaam.


Madam Rita, akimkumbatia chiby Dayo kama ishara ya kumuaga mara baada ya kazi ngumu ya kurekodi kipindi hicho.


Mmoja wa washiriki wa shindano hilo, Waziri Salum (kulia), akiwa amemkumpatia Chiby Dayo huku akiangua kilio baada ya rafiki yake mmoja kati yao kuyaaga mashindano hayo katika zoezi la kurekodi kipindi hicho lililokuwa likiendelea.


Waziri, aliendelea kulia kwa machungu huku akibembelezwa na Chiby Dayo.


Mmoja wa makamera man, waliokuwa wakiandaa kipindi hicho akiwajibika.


Majaji wa shindano hilo, Madam Rita (katikati), Salama Jabir kulia, na Master J, wakifuatilia mpambano huo kwa makini zaidi.


Jaji mkuu wa shindano hilo Madam Rita, akiongea jambo kwenye mchakato huo.


Washiriki walioingia kwenye tano bora wakiwa kwenye pozi la pamoja.


Watangazaji wa kipindi hicho Godwin Gondwe (kushoto), wakijadiliana jambo na Bob Junior, wakati wa kurekodi kipindi hicho.


Mshiriki wa kinyang'anyiro hicho Bella Kombo, akionyesha uwezo wake wa kuimba mahali hapo.


Bella Kombo, akionyesha uwezo wake.


Bella Kombo, kazini.


Mshiriki wa shindano hilo Rogers Lucas, akikung'uta gitaa mahari hapo.


Chiby Dayo akiwajibika.


Rogers Lucas, akionyesha ulaini wa nyonga yake jukwaani.



0 comments: