Social Icons

Saturday, May 28, 2011

VIMWANA 10 WATINGA FAINALI YA KIMWANA MANYWELE TWANGA PEPETA

Baadhi ya washiriki wa kinyang’anyiro hicho, wakiwajibika stejini.

HATUA ya nusu fainali ya kumsaka Kimwana Manywele Twanga Pepeta 2011, usiku wa kuamkia leo imefana vilivyo ndani ya Club Sun Cirro Shekilango, Dar es Salaam.
Katika mchujo huo, vimwana 10 wamechaguliwa kuingia fainali inayotarajiwa kufanyika Juni 17, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar.
Tukio hilo lilipambwa na burudani kabambe kutoka kwa Bendi ya The African Stars International ‘Twanga Pepeta’ na Kundi la Off-Side Trick.



Waimbaji wa Twanga Pepeta wakipamba shindano hilo kwa kuimba.


Msanii wa Kundi la Off-Side Trick, (kushoto), akikamua kwenye shindano hilo sambamba na mnenguaji wao.


Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka (kushoto) akiwa kwenye pozi na wageni waalikwa.



Mwimbaji mahiri wa Twanga Pepeta, Charles Gabriel ‘Chalz Baba’ ‘akirap’ kwa staili yake.


Asha Baraka (kushoto), akiteta jambo na mratibu wa shindano hilo, Maimartha Jesse.


Baadhi ya majaji wa shindano hilo wakiwa ‘bize’ na kazi yao.


Mashabiki waliohudhuria shindano hilo wakishuhudia kwa makini.


Mnenguaji wa Twanga Pepeta, Lilian Tungaraza ‘Internet’ akizungusha nyonga muda mfupi baada ya kuombwa kucheza pamoja na Kundi la Off-Side Trick.


Maimartha (kulia), akimkaribisha Asha Baraka azungumze machache kabla ya washindi kutajwa.


Vimwana Manywele Twanga Pepeta waliofuzu kuingia fainali wakiwa kwenye pozi la pamoja na baadhi ya viongozi wa shindano hilo.


Wanenguaji wa kike wa bendi hiyo, wakiwajibika jukwaani.

0 comments: