Social Icons

Tuesday, May 31, 2011

Banda la TA Reading latingisha ndani Ya Reading Carnival

Banda la TA Reading lilikuwa hivi.
Naibu Balozi wa Tanzania Uingereza, Chabaka Kilumanga (wa tatu kulia) akiwa na wadau wa Reading wakati wa Carnival.

URBAN PULSE CREATIVE inawaletea picha za matukio ya Reading Carnival iliyofanyika jana Jumatatu ambapo ilikuwa ni siku ya 'Bank Holiday'. Kwa mara ya kwanza TA Reading ikishirikiana na TANZ UK waliandaa banda la Kitanzania kwa kupika chakula cha Kitanzania na kuuza kwa wadau mbalimbali waliojitokeza kutembelea banda la TA ikiwa ni mojawapo ya mradi wa kuchangia mfuko wa TA Reading. Mgeni rasmi alikuwa Mh. Naibu Balozi wa Tanzania Uingereza, Chabaka Kilumanga aliyeambatana na Afisa wa Ubalozini Amosi Msanjila. Kwa ujumla banda ka Kitanzania lilitia fora kuliko mabanda yote mengine ya mataifa mbalimbali.
Zifuatazo ni picha zaidi za tukio hilo:

Afisa wa Ubalozi, Amosi Msanjila (kulia) akiwa na mpwa wake ndani ya Carnival.


Dello akiandaa kuku wa kuchoma.


Mdau Paul Onyango kutoka Bongo Fleva (kushoto) akiwa na wadau wa Reading.


Mh. Naibu Balozi Kilumanga (kulia) akijitayarisha kuchukua msosi.


Mpaka watasha walipagawa na banda la Kibongo.


Timu ya Urban Pulse ndani ya banda la TA Reading.


Wadau wa Reading wakila pozi ndani ya banda na TA Reading wakiwa na Berry Black (mwenye sweta nyekundu).


Nyomi iliyokuwepo pande hizo.

Asanteni

URBAN PULSE CREATIVE

0 comments: