Social Icons

Thursday, March 24, 2011

SERENGETI YAIMWAGIA TAIFA STARS MILLION 100

KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL), imetoa sh. milioni 100, kusaidia timu ya Taifa, Taifa Stars katika mechi ya timu hiyo na Afrika ya Kati, kesho kwenye Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. Pichani, Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo, akimkabidhi mfano wa hundi ya fedha hizo Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF), Angetile Oseah, katika Ofisi za TFF mjini Dar es Salaam, leo. Mbele ni Kocha mkuu wa Stars Jean Poelsen na wachezaji wa timu hiyo, Nahodha, Shadrach Nsajigwa na Mshambuliaji, Athumani Machupa.

0 comments: