Social Icons

Friday, February 4, 2011

WANAFUNZI WA CHUO CHA USAFIRISHAJI DAR WAMZUIA MKUU WILAYA YA KINONDONI KUINGIA CHUONI .

Baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wakiwa wametanda getini kuwazuia polisi kuingia chuoni hapo.

WANAFUNZI wa chuo cha usafirishaji (NIT) kilichopo Mabibo jijini Dar jana walimzuia mkuu wa wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana kuingia chuoni wakisema wamechoshwa na dharau za wakuu wao wa chuo na walimtaka mkuu huyo wa wilaya kwenda chuoni hapo na waziri husika ili kujadili matatizo yao.

Hata hivyo, baada ya majadiliano, Rugimbana aliruhusiwa kuingia chuoni hapo ambapo wanafunzi, wakiongozwa na rais wa serikali yao, Seif Khamis, walielezea matatizo yao wakitaka yatatuliwe mara moja .



Magari ya viongozi wa Wilaya ya Kinondoni yakiwa nje baada ya kuzuiwa kuingia chuoni.

Rais wa chuo hicho, Seif Khamisi (kulia), akiainisha mbele ya mkuu wa Wilaya Jordan Rugimbana (wa tatu kulia) na viongozi wa serikali kilichowafanya wagome.

Moja ya mabango yaliyokuwa getini likiwa na ujumbe wa kumkataa kaimu mkuu wa chuo hicho.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana, akiongea na wanafunzi muda mfupi baada ya kuruhusiwa kuingia katika ukumbi wa chuo hicho.

0 comments: