Social Icons

Monday, January 31, 2011

AROBAINI YA DOKTA REMMY YAFANA


Familia ya Dokta Remmy wakiwasha mishumaa

Leo Januari 29 ni siku ya arobaini ya mwanamuziki galacha hapa nchini, Ramazan Mtoro Ongala ‘Dokta Remmy’ iliyofanyika nyumbani kwake Sinza na baadaye baadhia ya watu waliohudhuria walikwenda kufanya maombi katika kanisa la Christian Centre Sinza Palestina.
Baada ya zoezi hilo, walikwenda makaburini kwa ajili ya kuwasha mishumaa na kuweka mashada.



Mtoto wa marehemu aitwae Godfrey akigawa shada la maua kwa ndugu zake.


Mzee Makasi aliyevaa miwani akiongoza sala (katikati kushoto) ni mke wa marehemu, Toni na mtoto wake Godfrey.



Mtoto wa marehemu aitwae Amani mwenye ulemavu na wenzake wakifuatilia mambo yaliyojiri kwenye shughuli hiyo.


Watoto wa marehemu wakitupia kokoto juu ya kaburi.


Mke wa marehemu aliyevaa nguo nyeusi akitoa shukrani kwa waliohudhuria

0 comments: