Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akielekea kukagua gwaride la maadhimisho ya sherehe za Uhuru zilizofanyika leo katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam
Katika maadhimisho hayo, Rais Kikwete, alikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na vikosi vya ulinzi na usalama ambavyo ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Mkuu wa Jeshi la Magereza Tanzania, Augustino Nanyaro akiwa amesimama na Mkuu wa gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama wakisubiri kupokea viongozi mbalimbali wa serikali.
Kamamda wa Kanda maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova, akiwekwa sawa na mlinzi wake tayari kwa kupokea wageni waalikwa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Magereza Tanzania, Augustino Nanyaro mara baada ya kuwasili uwanjani hapo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda, akiwasili kuungana na wageni waalikwa kwenye sherehe hiyo.
0 comments:
Post a Comment