Social Icons

Thursday, December 9, 2010

MGONJWA HOI BARABARANI


Joseph akiwa amelala barabarani ambako baadaye wananchi walifika na kumsaidia.

JAMAA mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Joseph, leo asubuhi alikutwa na kamera yetu akiwa ameanguka katika Barabara ya Forest mjini Morogoro, pembezoni mwa uzio wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Morogoro, akidai kwamba alikuwa ametokea katika hospitali hiyo na kwamba hali yake ilikuwa imezidi kuwa mbaya.
Akizungumza na mtandao huu, Joseph alisema: "Nimetoka humu ndani (hospitali) kutibiwa na baada ya kupewa dawa niliruhusiwa kurudi nyumbani, nilipofika hapa nimezidiwa na njaa pamoja na ukali wa dawa hizo na kujikuta nikiishiwa nguvu na kuanguka.
Kama kuna mtu ana shilingi elfu moja anisaidie nikanunue walau uji," alisema Joseph huku akionekana akitetemeka kwa njaa pamoja na ukali wa dawa hizo.

Alipoulizwa anasumbuliwa na ugonjwa gani alidai ni homa ya matumbo (typhoid) iliyoambatana na homa kali.
Mwandishi wetu alimpatia kiasi hicho cha fedha ambapo pia baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo walimuunga mkono mpiga picha wetu kwa kumuongezea kiasi cha fedha na baadaye kumwinua hadi kwenye mgahawa uliopo jirani na Shule ya Sekondari ya Morogoro.
Baada ya kupata hudumu hizo, Joseph alizinduka na kauli yake ya kwanza ilikuwa ni kuushukuru mtandao huu na wananchi wengine kwa kumpatia msaada huo.

0 comments: