Social Icons

Sunday, November 28, 2010

T- PAIN ALIVYO WAPAGAWISHA MASHABIKI BONGO!!

Dancehall kutoka Jamaica, Windel Benetol Edward “Gyptian” akifanya vitu vyake jukwaani wakati wa STR8 Muzik Festival Inter-College Special 2010 katika viwanja vya Posta Kijitonyama Dar es Salaam jana na kudhaminiwa na kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya SM.
Mwana Hipi Hop kutoka nchini Marekani , Faheem Rasheed Najm, “T-Pain” akitumbuiza wakati wa Tamasha Maalum la STR8 Muzik Festival Inter-College Special lililofanyika katika viwanja vya Posta Kijitonyama Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana na kudhaminiwa na kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya SM.


Baadhi ya wanenguaji wa T-Pain wakionyesha Swagger zao
T-Pain akimwaga Swagger zake kwa mashabiki waliofurika ndani ya viwanja hivyo.
Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Shawn Mims “Mims” akishambulia jukwaa.

Joh Makini akikamua katika tamasha hilo.
C Pwaa , akitumbuiza jukwaa wakati wa Tamasha Maalum la STR8 Muzik Festival Inter-College Special 2010 lililofanyika katika viwanja vya Posta Kijitonyama Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

C Pwaa akiwajibika na vijanawake jukwaani hapo.
Baadhi ya mashabiki wakishangilia baada ya kupagawishwa na wanamuziki waliokuwa wakitumbuiza katika Tamasha hilo.
Baada ya kutoka katika tamasha hilo Mateja20, ilitembele pande za Kinondoni katika Ukumbi wa Mango Garden, ambako Bendi ya African Stars International 'Twanga Pepeta' walikuwa wakimwanga burudani zao na kubahatika kumnasa Mwanamuziki kutoka nchini Kongo Bozi Boziana akifatilia kwa makini shoo ya Bendi hiyo.
Bozi Boziana akiangalia jinsi nyonga za watoto wa Asha Baraka, zilivyokuwa zikizungushwa. (kulia kwake), ni baadhi ya wanenguaji wake wakifuatilia makamuzi hayo kwa pamoja.
Kevi, wa pili kushoto akiwa kwenye pozi na washikaji zake katika shoo ya T- Pain, iliyofanyika katika Viwanja vya Posta jijini Dar, usiku wa kuamkia leo.
Muba (kulia), akiwa kwenye pozi na marafiki zake ndani ya ukumbi wa Mango Gardeni jijini Dar es Salaam.
Khaleed Chuma 'Chokoraa' (Kulia), akimnong,oneza jambo Pedeshee Bitus muda mfupi baada ya kukutana ndani ya ukumbi wa Mango Garden.
Pedeshee Bitus (kushoto) akimsikiliza kwa makini Chokoraa.
Viburudisho vikiwa kwenye pozi makini katika shoo ya T-Pain iliyofanyika ndani ya Viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Miss Bagamoyo 2010 Winifrida David (kulia), akijimiminia kilaji kwa kwenda mbele.

0 comments: