Social Icons

Wednesday, October 27, 2010

MPOTO ATOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA

Mpoto akigawia soda watoto yatima.

MSANII ‘first class’ katika miondoko ya mashairi nchini, Mrisho Mpoto a.k.a Mjomba, ametoa misaada kwenye kituo cha watoto yatima na wasio na makao maalumu, CHAKUWAMA Orphanage Centre, kilichoko Sinza-Mori, jijini Dar es Salaam ambacho kinamilikiwa na Mama Hadija.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mpoto alisema ameamua kuwasaidia watu hao akiamini kuwa ni jamii yake kwani yeye pia ni yatima na siku ya leo ni siku ya kuzaliwa kwake inayoambatana na tarehe ya kifo cha mama yake mzazi.

“Nimeamua kutoa misaada kwani ni sehemu ya kutambua uwepo wa kundi hili muhimu, hata mimi ni mwenzao kwani sina wazazi na kwa kuwa leo ni siku ya kuzaliwa kwangu na ni siku ambayo mama yangu mzazi alifariki. Hivyo katika hili sina cha kuongeza zaidi ya kuwatia moyo na Mungu atawalinda,” alisema Mpoto.

Mpoto ni msanii aliyepata mafanikio makubwa kutokana na mashairi yake na sasa ameweza kutengeneza bendi yake binafsi inayofahamika kwa jina la ‘Mjomba Band’ yenye makazi yake Kinondoni-Mkwajuni jijini Dar.


….Mpoto akiingia ndani ya mjengo wa watoto yatima.


….Akiongea Mama Hadija mmliki wa kituo hicho.


...Mama Hadija akimsikiliza Mpoto.



…. Akipokea misaada ya chakula na mafuta.


...Mpoto akitoa shukrani kwa Mama Hadija.


….Akijiandaa kuimba nao wimbo wa ‘Mjomba’.


....Tayari wimbo wa ‘Mjomba’ umeanza.


...DJ Choka naye alikuwepo.


...Ubao wa kituo hicho.


...Wimbo umekolea.


...Mjomba akiongea na waandishi wa habari.


...Mama Hadija akijibu maswali ya waandishi wa habari.


…..Akifurahi na watoto.

0 comments: