BAADA ya kupotea kwenye game ya muziki wa kizazi kipya kwa takribani miaka kadhaa, familia iliyowahi kufanya vyema katika tasnia hiyo, Hotpot Family imerudi upya ikiwa na sura tofauti huku waasisi wake wakiwa na maneno kadhaa ya kuongea.
Akipiga stori na Mateja20 kiongozi wa familia hiyo, Anselem Typhone Ngaiza ‘Soggy Dog’ alisema kwamba walichokifanya hivi sasa ni kuirudisha familia ikiwa katika muonekano mpya ili kuwapa nafasi chipukizi wanaoibuka waweze kuonekana. “Unajua siku hizi chipukizi wanapewa nafasi kubwa kuliko sisi wakongwe, ndiyo maana tunakuwa kimya, siyo kwamba sina kazi, nina ngoma kibao ndani lakini sizitoi kwa sababu hiyo, sijajua ni kwanini wadau wanafanya hivyo. Ndiyo maana tumeamua kutoka na vijana. “Mimi na Suma G kama wakongwe japo hatupewi heshima hiyo tumewapa nafasi kubwa wasanii wanaotoka kupitia Hotpot Family kwenye ngoma tuliyoiachia hivi karibuni ikiwa na jina la Wanamipango iliyofanyika Makavell Records,” alisema. Kwa upende wake Suma G alisema na safu hii kwamba, Hotpot Family ilikuwa inajipanga na sasa ndiyo kipindi chao cha ‘kushaini’ kwakuwa wamerudi tofauti huku wakiwa na nguvu mpya kutoka kwa vichwa kama Another One, Young Page, Baby Baby, Chorus B, na Blast Salim.
0 comments:
Post a Comment