Social Icons

Tuesday, August 2, 2011

RIHANNA AANIKA MAUMBILI KWA WAZAZI WAKE

Mwanamuziki mwenye mvuto kwa sasa, Rihanna, yuko nchini Barbados ambako ndiko nyumbani kwao akiuangana na wakazi wa visiwa hivyo kusherehekea mwisho wa msimu wa mavuno (Crop Over Festival), sherehe ambazo zinajulikana pia kama The Grand Kadooment na Rihanna akiwa balozi wake.


Kikubwa kilichojiri katika sherehe hizo zilizofanyika mapema leo, ni jinsi mwanadada huyu alivyo 'mwaga lazi' hadharani kwa kukata mauno wakati akicheza ngoma ya kwao ya Bajan huku akiwa amevaa kuvaa kimitego kama anavyoonekana katika picha hizi ambazo hivi sasa ni gumzo mtandaoni. Rihanna, ambaye hivi sasa anasumbua kwenye ulimwengu wa muziki na kibao chake matata cha Man Down, alionekana ku enjoy sherehe hizo kupita maelezo, kwani licha ya manyunyu ya mvua yaliyodondoka wakati fulani, hakuonekana kujali zaidi aliendelea kujichanganya huku akiwa na kinywaji chake cha asili mkononi! Hiyo ndiyo the Other side of Rihanna bwana!

0 comments: