Social Icons

Saturday, February 5, 2011

SANGOMA MTOA MAPEPO MORO


Pembe kubwa linalodaiwa kutolewa nje ya nyumba ya mkazi mmoja wa Mtaa wa Mtoni mjini Morogoro na Sangoma huyo.
MGANGA wa jadi (sangoma) anayefahamika kwa jina moja la Dk. Muzinga, jana jioni alitoa pembe kubwa nje ya nyumba ya mkazi mmoja wa Mtaa wa Mtoni mjini Morogoro, Bw. Said Ally (mwenye T-shirt ya Salama).

Akizungumza na matandao huu, sangoma huyo kijana alidai kwamba alipokea maombi kutoka kwa Bw. Ally akitaka nyumba yake ifanyiwe uchunguzi.

"Baada ya mteja wangu kuhisi mambo tofauti kwenye nyumba yake, alikfika hapa ofisini kuomba huduma yangu. Nilifika kwake na kioo changu kikanionyesha kwenye shimo lililo nyuma ya nyumba yake kwamba kuna pembe.

Nilipofukua nimelikuta hili pembe na nikaamua kuliteketeza na moto, " akasema Sangoma huyo.

Tukio hilo linaonyeshwa katika picha zifuatazo:


0 comments: