Social Icons

Thursday, November 25, 2010

PATCHO MWAMBA AMSHUKURU KIRUA!!

MWANAMUZIKI wa Bendi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' Patcho Mwamba, Hatimaye ameipua Single yake mpya inayokwenda kwa jina la Kirua.
Akiongea na Mateja20, hivi karibuni Patcho alisema kwamba amelazimika kufikisha shukrani zake kwa Pedeshee Mohamed Kirua, kwa njia ya wimbo kutokana na mambo mengi mazuri aliyomfanyia.
Patcho alisema kwamba tangu amekuwepo kwenye geme, kumekuwa na Mapedeshee wengi wanaomsapoti na yeye kuwapa shukrani zake lakini hajaona mwenye upendo na moyo wa kusaidia kama ilivyo kwa Kirua.
Single hiyo yenye ujumbe wa shukrani na sifa kende kede. Baada ya kukaa chini na kufiria sana namna ya kutoa shukrani hizo ambapo njia pekee aliona atumie sanaa yake ambayo pia itawafikia watu wengine wenye vipaji na sifa kama hiyo.


0 comments: