





WANAMUZIKI wanaounda Kundi la Mapacha wa Tatu,Khareed Chuma 'Chokoraa', Joseph Michael 'Jose Mara' na Junior Hamza 'Kalala Junior', mapema leo wametia timu katika ofisi kuu za MATEJA20 na kukutana na uongozi wa kampuni hii ambapo walielezea namna watakavyoweza kufanya uzinduzi wa Albam yao inayokwenda kwa jina la Jasho la Mtu.
Akiongelea uzinduzi huo meneja wa Mapacha Watatu Hamisi Dakota, alisema kwamba uzinduzi huo utafanyika Oktoba 15 mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Traver tine Magomeni jijini Dar es Salaa. Uzinduzi huo utasindikizwa na kudi zima la African Stars International ‘Twanga Pepeta Sugu Kisima cha Burudani' na Mfalme Mzee Yusuf.
Dakota aliongesa kwamba, albamu hiyo itakuwa na jumla ya nyimbo sita ikiwemo Private Case,Kipaji changu,Shika Ushikacho ambayo wamemshrikisha Mzee Yusuf,Mhudum,Nyumba ndogo na Imebaki Stori.
Dakota alitumia frusa hiyo kuwaomba mashabiki wao wote wahudhulie siku hiyo ili waweze kujionea staili adimu kutoka kwao.
0 comments:
Post a Comment