TANZANIA MODELS KUFANYA ONYESHO LA MAVAZI ARUSHA!!!
KIKUNDI cha Wanamitindo kijulikanacho kwa jina la 'Tanzania ModelsGroup' wanatarajia kufanya onyesho la mavazi katika ukumbi wa Via ViaClub jijini Arusha litakalofanyika jumamosi.Akizungumza na Dimba Mratibu wa onyesho hilo lililopewa jina la 'Timeand Beauty' Bi. Angel Justace alisema kuwa lengo la kuandaa onyeshohilo ni kuweza kutangaza umoja wao, kuvumbua vipaji vya vijana nakutangaza Utalii wa nchi ya Tanzania.Bi. Angel Justace alisema kuwa kwa sasa wakati umefika kwa vijanakuungana katika kutangaza utalii wa nchi."Sisi kama vijana hatuna budi kujitoa kwa kuungana na kutangazaaUtalii wa nchi yetu, kwani bila kufanya hivyo nchi yetu haiwezikutambulika na wageni hawawezi kujua nchi yetu ina vivutio ganivinavyovutia,"Onyesho hilo linalotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Via Via Clublitawakutanisha wanamitindo kutoka Dar es Salaam na jiji la Arushahuku wakipabwa na mbunifu wa mavazi ya asili Bw. Gabriel MollelSairiamu.Aliongeza kuwa mbali na mbunifu huyo wa mavazi ya asili Bw. GabrielMollel Sairiamu pia atakuwepo msanii wa kizazi kipya Hussein Machozi.Onyesho hilo limedhaminiwa na Hifadhi ya Taifa ya NgorongoroConservation-Arusha, Kilimanjaro Express Bus, Mwandago Evestiment,Coco Pazzo, Triple A Radio na Masai Club ya Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment