Social Icons

Saturday, May 22, 2010

DIAMOND MUSIC KILA IJUMAA MEEDA!

Bendi ya muziki wa Dansi nchini Diamond Music itakuwa ikitoa burudani kila siku ya Ijumaa ndani ya Ukumbi wa Meeda Club uliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.

Akitoa habari hii kwa msisitizo zaidi mkurugenzi mtendaji wa bendi hiyo Judis Moshi alisema kwamba tayari ameshakamilisha mazungumzo na uongozi wa Meeda kinachafuatia ni wao kuhakikisha wanaburudisha mashabiki wao kila siku ya Ijumaa.

Judis ametumia fursa hiyo kuwaomba mashabiki wake wote wajitokeze kwa wingi ili kutoa sapoti ya kutosha kwa bendi hiyo.

Rais wa Bendi ya Diamond Music Mulemle katikati akiongoza makamzi ya hatali na waimbaji wenzake ndani ya ukumbi wa Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo.

0 comments: