Social Icons

Tuesday, August 30, 2011

FUTARI YA KISOMO NA HITIMA YA JUMUIYA YA KIISLAMU NCHINI MAREKANI (TANZANIA MUSLIM COMMUNITY WASHINGTON DC YAFANA

Mgeni rasmi katika futari hiyo akitoa hutuba fupi ya kuwa pongeza na kuwashukuru viongozi pamoja na wana Jumuiya ya kiislamu Tanzania, na hotuba fupi ya kuhamasisha Watanzania waliokuwepo Marekani kujumuika na kusheherekea miaka 50 ya Uhuru wa nchi Tanzania.
Mgeni rasmi wa shughuli hiyo Balozi Mwanaidi Maajar, akiwa na waumini katika futari iliyoandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzania waishio nchini humo, kwenye ukumbi wa Hillandale Local Park, New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland Nchini Marekani.
Waumini wakipata futari ilioandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC
Waumini wa jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community wakiwa katika futari
Washauri waTanzanian Muslim Community Washngton DC, Jabiri Jongo katika picha ya chini na juu Mh Uwesu Bakar wakiwa katika dua ya kisomo cha kumuombea Marehemu Baba wa Dada yetu Jasmine Rubama, pamoja na kuwaombea jamaa zetu wote waliotangulia mbele. M/mungu awarehemu na awajaliee makazi meema peponi Amin.

Waumini wa dini ya kiislamu kwa upande wa wanawake wakiwa katika futari ya pamoja iliyofanyika jana jumapili Aug 28,2011 Silver Sring Maryland.
Dada yetu naye alihudhuria katika futari ya pamoja kwenye ukumbi wa Hillandale Local Park, mitaa ya New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland.
Ndugu jamaa na marafiki waliohudhuria katika kisomo pamoja na futari ilioandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community kenye ukumbi wa Hillandale Local Park New Hampshire Avenue,
Silver Spring Maryland.Saadie Fuad akipata flash ya pamoja na Amina Saleh katika futari ya pamoja
Waumini wa dini ya kiislamu kwa upande wa wanawake wakipata flash ya pamoja baada ya kumaliza futari ya pamoja iliyoandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community, katika ukumbi wa Hillandale Local Park New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland. Jana Jumapili Ramadhani ya 28, Aug 28,2011 picha zikiwa ni kama kumbukumbu ya Mwezi mtukufu wa ramadhani 2011 kutoka kwa mpiga picha wenu wa swahilivilla Editor Abou Shatry.
Dada yetu huyu naye alihudhuria katika futari ya pamoja kwenye ukumbi wa Hillandale Local Park, mitaa ya New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland.

0 comments: