Social Icons

Thursday, November 25, 2010

SENDOFF YA DADA 'AKE AUNT EZEKIEL YAFANA

Baadhi ya wanakamati wa shughuli hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja.

Usiku wa kuamkia leo pale pande za Victoria, katika Ukumbi wa Estana, kulifanyika Sherehe ya kumuaga Zawadi Ezekiel, ambaye ni dada yake na muigizaji wa filamu nchini Aunt Ezekiel. Sherehe hiyo ilianza majira ya saa 12:00 jioni na kumalizika mishare ya saa 6:30 usiku.
Kwa mjibu wa wageni waliohudhuria sherehe hiyo walisema kuwa walifurahishwa na maandalizi ya kamati tendaji na kwamba waliburudika vilivyo na hakuna sehemu iliyopwaya hata kidogo.
We' Sajenti kama vipi nyanyuka basi unisindikize ... si unajua nimepombeka kiana bwana eeh!!
Aunt Ezekiel (Kulia) akiwa na Dada yake Zawadi, ambae ni Bi. Harusi mtarajiwa, muda mfupi baada ya kumalizika sherehe hiyo.
Bi. Harusi akiwa kwenye pozi na baadhi ya wageni waarikwa.
Nice Chande akliomba msaada wa kunyanyuliwa baada ya kushindwa kubalansi viatu vyake.

Nice Chande akiwa kwenye pozi na Habiba.
The Great Kanumba akijiandaa kutupia mpunga na swahiba yake Ray katika sherehe hiyo.


Bi. Harusi akimrisha keki mshenga wake.
Aunt Ezekiel na wenzake wakizungusha nyonga .
Mayasa, akimkabidhi keki Bi. Harusi tayari kwa kuwakabidhi wazazi wake.
Johari (katikati), akibadirishana mawazo na wenzake aliyokuwa ameketi nao.

Mama Jesca (katikati), akifuatilia sherehe hiyo kwa makini zaidi.
Mc wa shughuli hiyo Maimartha Jesse akiongea jambo katika hafla hiyo.

0 comments: