Social Icons

Saturday, April 30, 2011

TIMU YA TAIFA YA TANZANIA CHINI YA MIAKA 23 YATUPWA NJE

Mchezaji wa timu ya Taifa ya Vijana ya Tanzania chini ya miaka 23, Thomas Ulimwengu (kushoto) akiambaa na mpira kumtoka beki wa wa timu ya Uganda (U 23) wakati wa mchezo wa marudiano wa kufuzu kucheza michuano ya All African Games inayotarajia kufanyika mwezi Septemba mwaka huu huko Msumbiji. Mchezo huo umechezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam,ambapo Uganda imeibuka na ushindi wa mabao 3-1.


HATA hivyo timu hiyo ya Tanzania imeshindwa kuutumia vyema uwanja wa nyumbani baada ya kulazimishwa kufungwa mabao 3-1 katika mchezo huo wa marudiano baada ya ule wa awali uliochezwa Nchni Uganda ambapo pia Tanzania ‘Manyara’ ililala kwa mabao 2-1.

Kwa hatua hiyo sasa Tanzania U23 imetupwa nje ya mashindano ya All African Games yanayotarajia kufanyika mwezi Septemba mwaka huu huko Msumbiji baad kukubali kufungwa jumla ya mabao 5-2.


Uganda ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika za mwanzo za mchezo huo na baadaye kuandika bao la pili na kufanya timu hizo kwenda mapumziko huku Uganda ikiwa mbele kwa mabao 2-0.


Kipindi cha pili Mbwana Samatta aliwainua mashabiki baada ya kuifungia timu yake bao 1 na la kufutia machozi kabla ya Uganda kufunga bao la 3 na la ushindi lililozima ndoto na matumaini ya watanzania ya kushinda mchezo huo.


Bao hilo ndilo hasa lilizamisha Jahazi la Tanzania na kuwafanya mashabiki lukuki waliojitokeza kushuhudia mchezo huo kuanza kuinuka vitini na kuanza safari za kurejea makwao.”TANZANIA UNDER 23 OUT MICHUANO YA ALL AFRICAN GAMES 2011”

0 comments: