Social Icons

Thursday, April 28, 2011

JANE MISO KUPANDISHWA KIZIMBANI

MWIMBAJI wa nyimbo za Injili anayetamba na Kibao cha Omoyo, Jane Miso (pichani), anatarajiwa kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuchikichia kiasi cha shilingi milioni kumi alizopewa kama mkopo na promota aliyefahamika kwa jina la Benson Mafuwe.

Akizungumza na mateja 20 pande za Mwananyamala, Dar es Salaam juzi, Mafuwe alisema kuwa kitu kinachomfanya kumfikisha mahakamani Jane ni kitendo chake cha kushindwa kuwa muungwana na kumtolea maneno ya vitisho.

“Nilidhani angekuwa muungwana na kuja tujue tunafanya nini, kumbe si hivyo, ndiyo kwanza alinipigia simu na kuanza kunitolea maneno ya kashfa, sasa mimi nataka mahakama iamue suala zima,” alisema Mafuwe.

0 comments: