Social Icons

Thursday, April 28, 2011

CHALZ BABA ANG’ANG’ANIA THE ATRIUMS

Chalz Gabriel Baba ‘Chalz Baba’ akipata msosi na shabiki wake, Isabela Godfrey mkazi wa Kinondoni Moroco jijini Dar ijumaa iliyopita.

MUIMBAJI katika Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Chalz Gabriel Baba ‘Chalz Baba’ Ijumaa ya wiki iliyopita alitoa mpya baada ya kugoma kuondoka kwenye Hoteli ya The Atriums iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar.

Kugoma huko kulitokana na kujiachia katika hoteli hiyo ya kifahari huku akiwa na shabiki wake, Isabela Godfrey mkazi wa Kinondoni Moroco jijini Dar.

Chalz Baba ‘alifuta’ wali na kuku mzima ambapo shabiki wake aliagiza Chips na kuku nusu huku kila mmoja akishushia grasi tatu za juisi aina ya pasheni ambapo huduma hiyo nzuri ndiyo iliyomsababishia muimbaji huyo kugoma kuondoka akidai aongezwe tena msosi kama ule alioletewa mara ya kwanza.

‘Siendi kokote yaani chakula kizuri namna hii mnanihudumia mara moja tu mbona nyinyi huwa mnaniandika mara kwa mara... siondoki hapa,’ alisema Chalz Baba.

Juhudi zakumtoa mwanamuziki huyo hotelini hapo zilifanikishwa na meneja mkuu wa hoteli hiyo kwa kumuahidi kumpa mwaliko siku si nyingi ili aje amalizie hamu yake.

Full kujiachia kwa Chalz Baba kulitokana na zoezi zima la Jiachie na staa linaloendeshwa na gazeti hili la kijanja na kudhaminiwa na hoteli hiyo ya kifahari.

Chalz Baba na shabiki wake huyo walifurahia huduma pamoja na mandhari nzuri ya hoteli hiyo ambapo muimbaji huyo aliahidi kwenda kusaka ‘mahela’ ili arudi kujinafasi katika ‘kiota’ hicho bomba kilichopo jijini Dar es Salaam.

0 comments: