Social Icons

Wednesday, December 29, 2010

UZINDUZI WA ALBAMU YA TID WAFANA BILICANAS

TID akionyesha makeke yake katika uzinduzi huo.
MWANAMUZIKI wa kizazi kipya, Khaleed Mohamed (TID), usiku wa kuamkia leo alifanya uzinduzi wa albam yake inayokwenda kwa jina la ‘Sifai’ ikiwa ni ya nne katika mfululizo wa albam zake. Uzinduzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Klabu ya Bilacanas na kuhudhuriwa na mashabiki wakiwamo mastaa kibao.

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Albert Mangwea ‘Ngwea’, akifanya makamuzi katika uzinduzi huo.

Mwanamuziki wa Hip Hop, Jaffary Mshamu ‘Jaffaray’ (kulia), akisalimiana na rafiki yake ambaye jina lake halikufahamika mara moja. Kushoto ni msanii wa filamu bongo, Chuchu Hans, akifutilia shoo hiyo.

Mshindi wa Big Brother 2009, Kevin Chuwang (kulia), akifuatilia uzinduzi huo na mchumba wake Elizabeth Gupta.

Kevin akionyesha uwezo wake wa kuchana mistari jukwaani katika uzinduzi huo.

Mmoja wa mashabiki waliofika ukumbini hapo akionyesha uwezo wake wa kukata nyonga.

Mwanamuziki Ambwene Yessaya ‘AY’ (kushoto), akikamua sambamba na TID.

0 comments: