Social Icons

Wednesday, December 29, 2010

LORI LA MAFUTA LA TEKETEA KWA MOTO MORO

Lori la mafuta likiteketea kwa moto eneo la Sangasanga, Morogoro.

LORI lililokuwa linasafirisha shehena ya mafuta ya petroli kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya, jana jioni liliteketea na moto kwenye msitu wa Mlima wa Mwarabu eneo la Sangasanga jirani na njia panda
ya kueleka Chuo Kikuu cha Mzumbe ambapo ni umbali wa kilomita 30 kutoka Morogoro
mjini.

Habari za awali zilizopatikana eneo la tukio zilidai kwamba lori hilo liliteketea baada ya kupatwa na hitilafu
ya umeme. Katika hatua nyingine, maafande wa kikosi cha Zima-Moto mkoa wa Morogoro, walizidiwa nguvu na moto huo baada ya magari yao mawili kuishiwa
maji huku moto huo ukiendela kuliteketeza gari hilo.

Tukio hilo ambalo lilivuta nadhari za watu wengi na kukwamisha kwa muda mrefu usafiri katika barabara hiyo, linaonekana katika picha ambazo zilinaswa na mtandao huu.

0 comments: