Social Icons

Wednesday, December 29, 2010

KESI YA CHENGE YAMALIZIKA LEO!


Chenge akiwasili katika Mahakaman ya Kinondoni leo asubuhi kusikiliza hukumu yake.

Umati uliokuwa ukifutilia hatima ya Chenge uliokuwepo mahakamani hapo asubuhi.

Chenge akijitapa kiutani kuwa yeye ndiye “Rais wa Afrika” wakati akisubiri kusomewa hukumu. Kulia ni wakili wake, Simon Mponda.

Mke wa Chenge, Tina Chenge, (kulia) na ndugu zake, wakichekelea baada ya hukumu kutolewa.

Chenge akipongezana na mkewe baada ya hukumu.

Mke wa Chenge na ndugu wengine wakihesabu pesa kwa ajili kulipa faini.

Chenge na mkewe wakiondoka mahakamani hapo baada ya kesi kumalizika.

Awali, MBUNGE huyo wa Jimbo la Bariadi (CCM), alitiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa makosa manne, mawili yakiwa ya uzembe, mauaji na kuendesha gari lisilokuwa na bima na kuhukumiwa kulipa faini ya shilingi laki saba
baada ya kupatikana na hatia kwa makosa yote au kwenda jela mwaka mmoja
kwa kila kosa. Baada ya hakimu aliyekuwa akiendesha kesi hiyo, Kwey
Lusema, kutoa hukumu hiyo, upande wa mshitakiwa ulijikusanya na kulipa
faini hiyo na kuondoka na ndugu yao.

0 comments: