Social Icons

Wednesday, November 10, 2010

TOP BAND NA MAKAMUZI YA BILICANAS USIKU WA KUAMKIA LEO

TID (kushoto) akimchezesha sebene mmoja wa mashabiki zake aliyejitokeza jukwaani.
Abubakari Mzuri akiwajibika stejini.
Mzuri (kushoto) akimchombezea 'song' jukwaani mrembo.
Mnenenguaji wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Asha Said 'Shalapova' akikatiza jukwaani muda mfupi baada ya kumtunza vijisenti Cha'z Baba.
TID na Abubakari Mzuri wakimchombeza shabiki wao.
Cha'z Baba akimimina song muda mfupi baada ya kuombwa kusalimia kisanii Club hapo.
Mwanamuziki wa Top Band Alawi Junior akisakata Rhumba kwa bidii.
Alawi akicheza staili ya mgongomgongo.
TID akiruka kwanja stejini.
Jose Mara (kushoto) akimsikiliza kwa makini Cha'z Baba mara baada ya kukaribishwa kutumbuiza kundi la 'mapacha watatu'
Cha'z Baba akionyesha Swagger zake kwa Daudi muda mfupi baada ya kushuka kuimba jukwaani.
Abubakari Mzuri akiwajibika stejini.
Mmoja wa wanamuziki wa Top Band akifanya makamuzi.
TX Junior (kushoto) akimtishia kiwiko Daudi ndani ya ukumbi wa Club Bilicanas usiku wa kuamkia leo.
Mrembo naye hakuwa nyumba kuunda pozi za picha Club hapo.

KUNDI la muziki la Top Band inayomilikiwa na Khaleed Mohamed ‘TID’ usiku wa kuamkia leo ilifanya shoo ya uhakika ndani ya ukumbi wa Billicanas Club jijini Dar es Salaam ambapo ilihudhuriwa na kundi la wanamuziki wa ‘Mapacha Watatu’ ambao pia walipata nafasi ya kutumbuiza kwa kibao chao cha ‘Kuachwa’.
Akiongea na paparazzi wetu ndani ya klabu hiyo, TID alisema kwamba bendi hiyo itakuwa ikifanya shoo zake kila siku ya Jumanne ndani ya ukumbi huo hivyo aliwaomba mashabiki wake waendelee kumsapoti kila ifakapo siku hiyo.







0 comments: