Social Icons

Wednesday, August 31, 2011

WAISLAMU KOTE DUNIANI WASWALI SWALA YA EID EL FITR LEO

LEO ni sikukuu ya Eid El Fitr ambapo waislamu kote duniani wamekusanyika katika misikiti na kuswali mara baada ya kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, ikiwa ni moja ya nguzo tano za dini ya kiislamu. mara baada ya kumalizika mfungo wa mwezi wa ramadhan waislamu hufanya ibada na kusherehekea kwa mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukumbushana mambo muhimu yanayohusu dini ya kiislamu.
Kama wanavyoonekana katika picha ni waumini wa dini ya kiislamu wakiswali katika msikiti wa Mtoni kwa Kabuma wilayani Temeke jijini Dar es salaam.
Hapa wakiswali kwa kusujudu.
Samaki mkunje angali mmbichi watoto wakitoka kuswali msikitini huku wenzao wakiwaangalia.
Vijana mbalimbali wakirejea nyumbani mara baada ya swala ya Eid asubuhi hii.
Asubuhi hii pilikapilika mbalimbali barabarani waislamu wakienda kuswali misikitini.
PICHA/HABARI NA FULL SHANGWE

0 comments: