Social Icons

Tuesday, August 30, 2011

CARNIVAL BABUKUBWA KATIKA MABALA YA ULAYA YAFANA

Msafara wa maandamano ukizunguka katika kitongoji cha Notting hill.
URBAN PULSE CREATIVE wakishirikiana na Miss Jestina Blog wanatujuza matukio katika picha ya 'Notting hill Carnival' iliyofanyika Jumapili tarehe 28 agosti 2011. Hii ilikuwa siku ya kwanza Carnival ya watoto ambayo hufanyika kila mwaka tangu mwaka 1964 ambayo siku ya pili inafuatiwa na siku ya watu wazima.

Maelfu ya watu zaidi walijitokeza katika mitaa ya Notting hill wakati wa Carnival hiyo ambayo ni tofauti na miaka yote pia iliyokuwa na usalama wa polisi 1000 wa ziada na kufanya Jumla ya polisi kufikia 6500, kwa ajili ya usalama na kufanikisha shuguli nzima ya wanachi walio hudhuria.

Hii inatoka na maasi yaliyo tokea hivi karibuni katika kitongoji cha Tottenham na sehemu nyingine nchini Uingereza.
Jumla ya watu 53 wanashikiliwa na polisi kutokana kutaka kufanya fujo katika carnival hiyo.












0 comments: