Social Icons

Monday, August 29, 2011

TWANGA KUTUMBUIZA SIKUKUU YA IDDI MANGO GARDEN


BENDI ya Muziki wa dansi chini ya The African Stars International 'Twanga Pepeta Sugu Kisima cha Burudani', katika sikukuu ya Iddi mosi, wanatarajia kufanya maonesho yake ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mateja20, makao makuu ya ofisi za Bendi hiyo Kinondoni jijini Dar Meneja wa bendi hiyo Hassan Rehani alisema, katika sikukuu hiyo Twanga pepeta itatoa burudani zake ndani ya Ukumbi huo mchana na usiku na kesho yake watakuwa ndani ya Ukumbi wa TCC Club Chang'ombe.

"Burudani zetu zote zitaishia hapo siku ya sikukuu Iddi na 4/09/2011, tutakua ndani ya Ukumbi wa Msasani Beach Kawe jijini Dar es Salaam, katika shoo maalum", Alisema Hassani.

0 comments: