Social Icons

Tuesday, April 26, 2011

BONGO MOVIE WASHINDWA KUTETEA JINA LAO KWENYE BONANZA LA PASAKA TABATA

Mwandaaji wa Bonanza hilo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Paris Pub, John Mange (kulia), akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya Long Room, kwenye hafla fupi ya utoaji zawadi hizo, iliyofanyikwe kkatika eneo la Paris Pub.
Bendi ya Extra Bongo, Wazee wa mjini Mipango, wakitumbuiza kwenye Bonanza hilo.
Mmoja wa Wanenguaji wa bendi hiyo akionyesha uwezo wake.
JB, akidokezwa na viongozi wake namna atakavyofanya mara baada ya kuvaa jezi tayali kwa kabumbu.
Beny Kinyaiya, akipasha misuli na JB
JB, akipasha msuli muda mfupi kabla ya mechi yao kuanza.
Baadhi ya mashabiki waliofulika, Viwanjani hapo wakifualia mechi hizo kwa makini.
Dokta Cheni, akisepa mdogo mdogo, mara baada ya timu yao kufungwa.
Papa B2C, akikabizi zawadi kwa washindi wa pili.
Papa B2C, akiongea jambo kwenye hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo, iliyofanyika eneo la Paris Pub Tabata.
Mkurugenzi wa Paris Pub, John Mange, akiangalia zawadi za washindi wake.
Tinno (kulia), akitembea kwa unyonge muda mfupi baada ya mechi hiyo kumalizika
Muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Ruth Suka 'Mainda,' akiangalia kitu kwenye pensi ya mmoja wa wachezaji hao.
Baadhi ya mashabiki wa timu hiyo wakionekana wenye hudhuni mara baada ya timu yao kufungwa magoli mawili kwa bila

Wachezaji wa timu ya Bongo Movie wakipeana mawaidha muda mfupi baada ya mapumziko.
JB, akichachawa uwanjani hapo.

TIMU ya mpira wa miguu inayoundwa na baadhi ya mastaa kutoka ndani ya Tasinia ya Filamu Bongo, jana jumatatu ya Pasaka, walikuwa wamearikwa kwenye Bonanza la Paska, lililokuwa limeandaliwa na Mkurugenzi wa Paris Pub Bwana John Mange, katika Viwanja vya Shule ya Msingi Tabata jijini Dar es Salaam.


Katika Bonza hilo timu hiyo ya Bongo Movie, ilishindwa kufurukuta katika mechi zote mbili ilizokuwa imepangiwa na kujikuta ikiambulia patupu.

Hadi mwisho wa michuano hiyo timu ya Long Room, iliibuka kidedea na kukabidhiwa set ya Jezi na kleti tatu za bia.

0 comments: