Social Icons

Wednesday, March 30, 2011

YANGA WAIGALAGAZA AZAM FC

Kikosi kizima cha Yanga Enzi za kina Ambani.

TIMU ya soka ya Yanga mapema leop, imejiweka kwenye nafasi nzuri, baada ya kuigonga tmu ya Azam FC mabao 2-1 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Yanga inatalajia tena kukigonga na watetezi wa kombe hilo Simba SC hivi karibuni.
Katika mechi hiyo iliyokuwa na upinzani wa hali ya juu, iliwachukua wauza koni ‘Lambalamba’ Azam FC dakika mbili tu kucheka na nyavu za Yanga, baada ya John Boko ‘Adebayor’ kutupia wavuni shuti kali.
Dakika ya 9, Mrisho Ngassa alipiga shuti kali lakini likadakwa na kipa Ivan Knezevic, kabla ya Yanga kujibu kwa shuti kali la Davis Mwape lililogonga mwamba dakika ya 12, huku Jerry Tegete naye akikosa mabao ya wazi matatu kutokana na kupiga mpira fyongo.
Dakika ya 41 Gerson Tegete alijipanga sawa na kupachika bao la kusawazisha baada ya kumpiga chenga kipa na beki wa Azam, huku mwamuzi wa mchezo huo Said Ndege, akimzawadia kadi ya Jano Tegete.
Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, timu hizo zilitoka Uwanjani zikiwa zinasale ya 1-1.
Baada ya kulejea Uwanjani kwa ungwe ya pili, Tegete tena alipokea mpira na kupachika bao la pili kwa kichwa akitumia vema pasi ya Mwape na kumtoka kipa Nyonzikuru.

0 comments: