Social Icons

Tuesday, March 29, 2011

BAADA YA KUTEMWA TIMU YA TAIFA, MACHAKU AIBUKIA MCHANGANI

Mshambuliaji Salum Machaku (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa timu ya Black People wakati akiichezea timu ya Mikocheni jana jioni.


IKIWA ni siku chache zimepita toka Kocha Mkuu wa Taifa Stars Jan Poulsen kumtema mshambuliaji wa timu ya Mtibwa Sugar, Salum Machaku 'Sharobaro' katika kikosi chake kilichopambana na Afrika ya Kati kwenye mchezo wa kuwania kufuzu Fainali za Afrika uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es salaam na stars kuibuka na ushindi wa bao 2-1, mchezaji huyo jana jioni alinaswa na mtandao huu akicheza ligi ya mchangani katika uwanja wa shule ya msingi Mwembesongo akiichezea timu ya Mikocheni inayomilikiwa na wapiga debe wa stendi kuu ya mabasi ya Msamvu, Morogoro.

Hata hivyo 'staa' huyo licha ya kucheza kwa nguvu zake zote katika mchezo huo alimaliza dakika 90 bila kuifungia bao timu yake hiyo baada ya kubanwa vilivyo na 'Machalii' wa timu ya Black People yenye maskani yake ndani ya kilabu cha kuuza pombe za kienyeji kiitwacho Kaloleni cha Mji Mpya, ambapo katika mchezo huo wa ligi ya kugombea jezi inayojulikana kwa jina la 'Mwembesongo Cup' iliyoandaliwa na wadau wawili wa soka wa mkoani hapa, Daudi Juliani na Master Mage timu hizo zilitoka suluhu.

Mara baada ya mchezo huo kumalizika mwandishi wetu alizungumza na mchezaji huyo ambapo alidai kwamba kwa sasa yupo mkoani hapa kwa matatizo ya kifamilia na kwamba kuonekana katika ligi hiyo ni moja ya mazoezi.

0 comments: