Social Icons

Wednesday, March 30, 2011

TUTAKUKUMBUKA DAIMA HAIKA

Haika Robert Masue (32) hatunaye tena. Amefariki Jumamosi Machi 26, mwaka huu katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es salaam baada ya kushikwa na shinikizo la damu la ghafla. Amefariki ikiwa ni wiki chache zimepita tangu ajifungue mtoto. Haikal, ambaye alikuwa mfanyakazi wa kampuni ya wakala wa bima ya Agin Insurance Brokers, atakumbukwa kwa uchapakazi wake na pengo lake litachukua miaka mingi kuliziba, kwani utendaji wake wa kazi ulikuwa hauna mfano. Global Publishers inaweza kuthibitisha hilo kwa sababu alikuwa akihudumia magari ya kampuni na ya viongozi wake kwa ufanisi wa hali ya juu, alikuwa anaweka kumbukumbu vizuri na hakuna wakati alipitisha tarehe za Bima. Haikal anatarajiwa kuzikwa leo Moshi. Bwana alitoa, Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe. Mungu ailaze roho yake mahali pema - Amin

...wakitoa jeneza kutoka nyumbani kwa wazazi wa marehemu, Kitunda, Ukonga.

...kanisa la Kilithuri la Gongo la Mboto kulikofanyika ibada

...waombolezaji wakiwa kanisani. Katika ni mama wa marehemu

...waombolezaji wakimuaga marehemu

...wakiingiza jeneza kwenye basi tayari kwa safari ya kuelekea Moshi kwa maziko.

0 comments: