Social Icons

Saturday, February 19, 2011

WAHANGA WA MABOMU WAENDELEA KUFARIJIWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimfariji Mohamed Rashid Mkaazi wa Majohe mmoja kati ya majeruhi walioathirika na milipuko ya mabomu iliyotokea juzi usiku kwenye Ghala la kutunzia silaha katika kambi ya JWTZ Gongolamboto jijini Dar es salaam, wakati alipotembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili leo, kwa ajili ya kuwafariji majeruhi hao.

Saida Rajab (36) mkazi wa Ukonga Mombasa, akiwa amelazwa kwenye wodi ya Mwaisela Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kukatwa mkono na moja ya bomu lililosababishwa na milipuko ya mabomu yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye ghala la Silaa katika kambi namba 511 KJ ya Jeshi la Wananchi (JWTZ), Gongolamboto juzi.Agnela Mwangoma, ambaye pia ni mmoja kati ya majeruhi waliolazwa hospitali ya Muhimbili, akiwa amewekewa vyuma mkononi.

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, akimjulia hali mtoto Zuena Issa, mkazi wa Kitunda, aliyelazwa kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Baadhi ya Scout, wakibeba magodolo kupanga katika ukumbi wa PTA baada ya kufikishwa mahala hapo na wasamaliawema waliotoa msaada huo kwa ajili ya watoto ambao bado hawajaonana na wazazi wao, wanaoendelea kushi mahala hapo chini ya Red Cross.

Baadhi ya watoto ambao bado wapo katika ukumbi huo wakisubiri kuja kuchukuliwa na wazazi wao.
Watoto wengine walikuwa wakijifariji kwa kucheza kiduku kama mtoto huyu anavyoonekana akiwaburudisha wenzake.

Hii ni baadhi ya misaada iliyofikishwa katika ukumbi huo leo mchana.

Baadhi ya vijana wanaotoa huduma ya Scout katika ukumbi huo.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, akizungumza na watoto waliokusanywa katika Banda la PTA Sabasaba leo mchana, wakati alipowatembelea watoto hao waliopoteana na wazazi wao kutokana na mlipuko wa mabomu.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadiq, akizungumza na baadhi ya wazazi waliofika katika ukumbi wa PTA, ambao bado hawajawapata watoto na ndugu zao. Lakini idadi ya wazazi wanaoendelea kuwatafuta watoto wao inaonekana kuwa bado ni kubwa ukulinganisha na idadi ya watoto waliosalia katika ukumbi huo ambao ni jumla ya watoto 18 tu.

Wazazi walifika kutafuta watoto wao wakimkiliza Kamanda wa Polisi, Suleiman Kova.

Baadhi ya watoto hao wakipata msosi, ukumbini humo.

Picha: Sufianimafoto Blog...

0 comments: